Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amepatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp pasi na kukusudia
Akitoa uamuzi wake jaji Thokozile Masipa alisema kuwa mwanariadha
huyo alimuua Reeva kwa bahati mbaya alipofyatua risasi kupitia kwa
mlango wake wa choo akiwa akatika hali ya mshtuko akidhani kuwa jambazi
alikuwa amevamia nyumba yake.
Alisema kuwa upande wa mashitaka
umeshindwa kuthibitisha kuwa Pistorius alinuia kumuua Steenkamp na
kwamba alifanya mauaji hayo kwa kusudi.
Pia alipatikana na hatia ya kosa la kutumia silaha yake visivyo alipokwenda mgahawani.
Jaji Thokozile Masipa amesogeza muda wa mwanaridha huyo yuko huru kwa dhamana.
Pistorius
atakuwa huru hadi hukumu itakapotolewa mwezi ujao, ambapo anaweza
kuhukumiwa hadi miaka 15 gerezani. Oscar Pistorius ataendelea kukaa kwa
mjombake alikokuwa muda wote kesi ilipokuwa ikiendelea.
Mjombake Pistorius, Arnold Pistorius amemshukuru Jaji Masipa kwa uamuzi wake wa kumuachia kwa dhamana.
No comments: