Taarifa Kamili Kutoka Kwa Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma,David Misime Kuhusu Vipeperushi Vyenye Vitisho Vinavyosambazwa Mjini Dodoma
Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma,David Misime
WanaCCM
walifika katika jengo lao jana Alhamisi, Septemba 25, 2014, Dodoma na
kukuta limeandikwa maneno kwa rangi nyekundu "NO KATIBA UFISADI " na
kama hilo halitoshi kukawepo vipepersuhi vinasambazwa.Picha: Lukwangule
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID
MISIME - SACP amesema tarehe 25/09/2014 alfajiri vimeokotwa vipeperushi
maeneo mbalimbali mjini Dodoma vyenye ujumbe ufuatao:ONYO – DODOMA SI MAHALI PA KUFUGA WEZI WA FEDHA ZA UMMA. UTAKAYEINGIA BUNGENI KUANZIA KESHO, YATAKAYOKUPATA UTAJUTA.
Kamanda
MISIME amesema tumeendelea kupokea taarifa za watu wanaodaiwa kuandaa
vipeperushi hivyo na tunafanyia kazi ili tuweze kuwakamata ili
washtakiwe kulingana na kosa walilolitenda hasa la kutoa vitisho na
kuhamasisha uvunjifu wa amani.
Aidha
Kamanda MISIME ameongeza ametoa wito kwa wananchi na wageni wanaofika
Dodoma watii sheria bila shuruti. Kila mmoja ajiepushe kujiingiza kwenye
kuhamasisha uvunjifu wa amani, kujiingiza katika mikusanyiko isiyo
halali na maandamano ambayo yameshapigwa marufuku na Jeshi la Polisi.
Atakayekiuka
na kujiingiza katika vitendo hivyo vya kiuhalifu atashurutishwa kwa
nguvu zote kwa mujibu wa sheria za Nchi na kwa mamlaka iliyopewa Jeshi
la Polisi.
Kamanda
MISIME ameongeza kuwa wananchi na wageni wapenda amani waendelee na
shughuli zao kama kawaida kwani Jeshi la Polisi limejiimarisha ipasavyo
kukabiliana na yeyote yule atakayekiuka sheria na maelekezo
yaliyotolewa.
No comments: