TAARIFA: WANAJESHI WA 3 WA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA NA RAIA 1 WAFA KATIKA AJALI YA KIFARU MTWARA
Kifaru kilichokuwa kikisafiri kutoka Mtwara
kwenda Lindi kikiwa kimeacha njia na kugonga nyumba usiku wa kuamkia leo katika
kijiji cha Mnolela Lindi vijijini, kusababisha vifo vya watu watatu katika
ajali hiyo.Na Mpiga Picha Wetu
Ajali hiyo ilitokea katika Barabara ya Mingoyo, baada ya kifaru cha jeshi kugonga nyumba na kusababisha kifo cha Somoe Kamteule aliyekuwapo ndani. Pia askari mwenye namba Mt 10728 Pascal Komba alikufa katika ajali hiyo.
Gari hilo ni la Kikosi Namba 83, ambalo liliacha njia na kugonga nyumba mbili na raia na kusababisha vifo hivyo. Dereva wa gari hilo alikuwa askari Shandili Nandonde.
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga alisema ajali hiyo ilitokea
jana saa 11.30 alfajiri. Gari hilo lilikuwa likitoka mkoani Mtwara
kwenda Nachingwea.
Aidha
Kamanda huyo alitaja waliojeruhiwa ambao ni askari wa JWTZ kuwa ni
Simon Edward, Feruzi Hadji, Omary Makao, Mbaruku Duchi, Simon Masele,
Shadhili Nnandonde na mwingine aliyefahamika kwa jina moja Ndekenya.
No comments: