Wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram wameuzingira mji wa Maiduguri , mji rasmi wa jimbo la Borno Kaskazini Mashariki ya Nigeria.
Wazee wa vijiji wametahadharisha kuwa jeshi linahitaji kuweka ulinzi
thabiditi katika mji huo ambao una zaidi ya watu milioni 2 ili kuzuia
mashambulizi kutoka pande zote za mji huo.
Kundi hilo limeteka sehemu kadhaa ambazo ziko umbali wa kilomita 50 kutoka Maiduguri.
Kadhalika kundi hilo lilitangaza maeneo iliyoyateka kama himaya zao.
Serikali haijatoa tamko lolote kuhusu taarifa iliyotolewa na wapiganaji hao.
Kwingineko
wakaazi wa miji iliyozungukwa na Boko Haram Kaskazini Mashariki ya
Nigeria, wameelezea hatari kubwa inayowakabili wakati wamejipata
katikati mwa makabiliano kati ya wanajeshi wa serikali na wanamgambo
hao.
Baadhi waliokwama katika maeneo yenye milima wamelazimika kula majani kama chakula.
Kwa
siku kadhaa sasa jeshi limekuwa likijaribu kuwasamabaratisha wapiganaji
wa Boko Haram kutoka mji wa Michika - mji ambao ni wa hivi karibuni
kudhibitiwa na wanamgambo hao.
Katika mji wa Michika watu
wamekwama kati ya mabomu ya jeshi la wanahewa Nigeria na wapiganaji wa
jihadi wanaomfyatulia risasi mtu yoyote anayosogea, na kwa mara nyengine
hata kuwakata shingo waathiriwa.
Mwanamke mmoja ameiambia BBC kwamba watoto wengi wamekwama nyumbani mwake na hawajui wazazi wao waliko.
Miongoni
mwa walioukimbia mji huo na kwenda katika milima iliyo karibu, sasa
wameishia kula majani. Mwanamume mmoja amesema watu 7 wamefariki mahali
alipojificha, na hawawezi kuzikwa.
Wakati huo huo kundi la
viongozi wanaoheshimiwa wanasema Boko Haram wameulenga mji mkubwa
Kaskazini mashariki mwa Nigeria, Maiduguri.
Viongozi hao wa Borno
wanasema miji na vijiji vilivyouzunguka mji huo tayari vimedhibitiwa na
wanamgambo hao.Kundi hilo limeshutumu namna serikali inavyokabiliana na
hali.
Habari na BBCswahil.com
No comments: