KAMATI YA BUNGE LA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA YAENDELEA NA UKAGUZI KATIKA MIGODI
Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na
Mazingira imeendelea na ukaguzi katika Migodi ya dhahabu kufahamu utekelezaji
wa Sheri a ya Mazingira. Katika Mgodi wa Bulyanhulu Kamati iliangalia jinsi
maji yenye kemikali yanavyohifadhiwa na udhibiti wa taka za plastiki
mgodini hapo. Migodi iliyotembelewa
mpaka sasa ni Mgodi wa North Mara, Geita na Bulyanhulu. Hii leo Kamati hii
itaendelea na ziara yake katika mgodi wa Buzwagi.
Naibu
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu (wa pili kutoka kulia) akitoa
ufafanuzi wa kisheria mbele ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na
Mazingira. Kamati hiyo iko katika ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa Sheria
ya Mazingira katika Migodi. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Kamati ya
Bunge Mh. James Lembeli (wa tatu kulia), Mh. John Mnyika na Mh. Henry Shekifu
wajumbe wa Kamati hiyo. Wa kwanza (kushoto) ni Bw. Peter Burger, Meneja Mkuu wa
Mgodi wa Bulyanhulu.
Pichani
ni taka za plastiki zilizohifadhiwa vizuri kwa ajili ya urejelezwaji katika
Mgodi wa Bulyanhulu.
Wajumbe
wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira wakiwa katika picha ya
pamoja na Watendaji wa Mgodi wa Bulyanhulu wakati wa ukaguzi katika Mgodi huo
kuona utelekezaji wa Sheria ya Mazingira.
Wajumbe
wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira wakiwa katika picha ya
pamoja na Watendaji wa Mgodi wa Bulyanhulu mara baada ya ukaguzi katika Mgodi
huo kuona utelekezaji wa Sheria ya Mazingira.
No comments: