KUTOKA IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA RASMI BARABARA YA MWENGE-TEGETA JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mbunge wa Kawe Mhe Halima Mdee baada
ya ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo la
Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es salaam. Ujenzi na upanuzi wa
barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya
Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es
Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa
barabara ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe
jijini Dar es salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km
12.9, ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza
msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa barabara
ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar
es salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni
sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa
magari katika jiji la Dar es Salaam.
Wananchi
wakifurahia hotuba ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa ufunguzi
rasmi wa barabara ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda
ya Kawe jijini Dar es salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya
Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa
kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Wapiga picha wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwa tayari tayari
kumrekodi Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi wa barabara ya
Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es
salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni
sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa
magari katika jiji la Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada
wakifungua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa barabara ya
Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es
salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni
sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa
magari katika jiji la Dar es Salaam. Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Mhe Saidi Meck Sadiki, Meya wa Konondoni Mhe, Mbunge wa Kawe Mhe
Halima Mdee na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dar es salaam Ndg Ramadhani
Madabida
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada
wakifurahia baada ya kufungua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa
barabara ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe
jijini Dar es salaam. Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km
12.9, ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza
msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam. Wengine ni Mkuu wa
Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadiki, Meya wa Konondoni Mhe,
Mbunge wa Kawe Mhe Halima Mdee na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dar es
salaam Ndg Ramadhani Madabida
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada
wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwenge-Tegeta
leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es salaam.
Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni sehemu ya
mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari katika
jiji la Dar es Salaam. Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe
Saidi Meck Sadiki, Meya wa Konondoni Mhe, Mbunge wa Kawe Mhe Halima
Mdee, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Musa Iyombe na viongozi wengine
Sehemu
ya barabara ya Mwenge-Tegeta yenye urefu wa Km 12.9, ambayo ni sehemu
ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari
katika jiji la Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada
wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwenge-Tegeta
leo katika eneo la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es salaam.
Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni sehemu ya
mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari katika
jiji la Dar es Salaam. Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe
Saidi Meck Sadiki, Meya wa Konondoni Mhe, Mbunge wa Kawe Mhe Halima
Mdee, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Musa Iyombe na viongozi wengine
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada
baada ya ufunguzi rasmi wa barabara ya Mwenge-Tegeta leo katika eneo
la Lugalo njiapanda ya Kawe jijini Dar es salaam. Ujenzi na upanuzi wa
barabara ya Mwenge-Tegeta Km 12.9, ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya
Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadiki, Mbunge
wa Kawe Mhe Halima Mdee, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Musa Iyombe na viongozi wengine. PICHA NA IKULU
Jumatano, Oktoba
Mosi, 2014, amezindua rasmi Barabara ya Kisasa ya Mwenge-Tegeta ambayo ni
sehemu ya Barabara ya New Bagamoyo Road, mjini Dar Es Salaam.
Barabara hiyo yenye
urefu wa kilomita 12.9 imegharimu kiasi cha Sh. bilioni 77.85, fedha ambazo
zimetolewa na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo ya Kimataifa
la JICA. Serikali ya Tanzania imechangia asilimia 7.64 katika gharama za ujenzi
wa Barabara hiyo.
Rais Kikwete amefanya
uzinduzi huo katika eneo la Makutano ya Kambi ya Jeshi ya Lugalo na Barabara ya
Kawe katika sherehe iliyoshuhudiwa na mamia ya wananchi. Alikuwa ni Rais
Kikwete ambaye aliweke jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara hiyo Aprili 4,
mwaka 2011.
Barabara hiyo ni awamu
ya kwanza ya ujenzi wa Barabara itokayo Makutano ya Barabara ya Kawawa,
Kinondoni hadi Tegeta. Ujenzi wa awamu ya pili wa kilomita 4.3 kati ya Mwenge
na Makutano ya Barabara ya Kawawa, unatarajiwa kuanza wakati wowote baada ya
mipango yote ya ujenzi huo kukamilika.
Barabara hiyo ya
Mwenge-Tegeta inalenga kupunguza msongamano wa magari katika eneo la kaskazini
mwa Dar Es Salaam na pia ni sehemu ya bararaba kuu inayounganisha Jiji la Dar
Es Salaam na Mkoa wa Pwani, kupitia Wilaya ya Bagamoyo, na kuunganisha mikoa
hiyo na mikoa ya kaskazini mwa Tanzania.
Akizungumza kwenye
sherehe hiyo ya uzinduzi wa Barabara hiyo iliyojengwa na Kampuni ya Konoike
kutoka pia Japan, Balozi wa Japan katika Tanzania, Mheshimiwa Masaki Okada
amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulichelewa kukamilika mwaka jana, kama
ilivyopangwa, kwa sababu ya wajenzi kukabiliwa na matatizo ya mafuriko makubwa
yaliyotokea mwaka 2011.
Mbali na kutaja misaada
mingi katika sekta ya miundombinu na hasa barabara ambayo imefadhiliwa na Japan
katika miaka mingi iliyopita, Mheshimiwa Okada amesema kuwa Japan sasa iko
tayari kuanza ujenzi wa Barabara ya Gerezani-Bendera Tatu, Dar Es Salaam,
utakaogharimu Sh. bilioni 18.5, msaada kutoka Japan.
utakaogharimu Sh. bilioni 18.5, msaada kutoka Japan.
Aidha, Balozi huyo
amewaomba radhi Watanzania kutokana na ucheleweshaji wa kuanza kwa ujenzi wa
barabara ya juu kwa juu –flyover-
katika eneo la TAZARA, Dar Es Salaam, ambao utagharimu Sh. bilioni 53 ambazo
zinatolewa na Serikali ya Japan kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la
JICA.
Amesema kuwa ujenzi huo
umechelewa kwa sababu makandarasi wa Kijapan ambao walitakiwa kujenga flyover hiyo wanakabiliwa na kazi nyingi
huko nyumbani za kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa na tetemeko na kimbunga
cha Great East Japan Earthquake and Tsunami,
kilichotokea Machi 2011 na kusababisha uharibifu mkubwa mno.
Aidha, amesema kuwa
wajenzi hao pia wanalazimika kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha
miundombinu ya kuiwezesha Japan kuandaa Michezo ya Olimpiki ambayo imepangwa
kufanyika nchini humo mwaka 2020.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
1 Oktoba, 2014.
No comments: