Shirika la afya duniani leo linaongoza mkutano wa kamati yake ya dharura , kutathmini hali ya hivi karibuni kuhusiana na mlipuko wa Ebola
Mkutano huo unafanyika wakati ugonjwa huo ukiendelea kuenea katika
nchi tatu zilizoathiriwa zaidi na ugonjwa huo Guinea, Sierra Leone na
Liberia - ingawa Senegal na Nigeria, ambazo zilikuwa na visa vichache
zimetangazwa kutokuwa na ugonjwa huo.
Ni mara ya tatu sasa kamati ya dharura ya WHO inakutana .
Lengo la sasa ni kutathmini juhudi zilizofikiwa za kudhibiti ugonjwa huo na kuuzuia kuenea.
Shirika la afya duniani linakabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kuchelewa
kuzorota kuchukua hatua dhidi ya mlipuko huo , suala ambalo linaonyesha
kuwa hakuna ishara ya kupungua kwa maradhi hayo katika nchi za Liberia,
Guinea ama Sierra Leone.
Kamati hiyo itaangalia hatua zilizopo za
uchunguzi wa mlipuko huo katika mipaka. Je hatua hizo zinafaa, na je
yaweke masharti kamili ya kusafiri kwenye maeneo hayo ?
Kuna
baadhi ya sababu ndogo za kuwa na matumaini - kwa pamoja Nigeria na
Senegal zimeweza kuzuia kuenea kwa visa vya Ebola . Na awamu ya kwanza
ya kinga za majaribio zinazoweza kuaminika zinatarajiwa kuwasili Geneva
hii leo.
Lakini kinga kamili zilizoidhinishwa dhidi ya Ebola huenda zikapatikana miezi kadhaa ama baada ya mwaka
Habari na BBCswahili.com
No comments: