Ads Top

Inadaiwa kuwa wanunuzi, raia wa Uchina walinunua maelfu ya kilo za pembe za ndovu nchini Tanzania na kuzitorosha kutoka nchini humo katika ndege ya kibinafsi ya raia wa Uchina Xi Jinping,wakati alipozuru bara Afrika

 
 Rais Xi JinPing wa Uchina alizuru nchini tanzania mwaka uliopita
 
Kulingana na shirika la ujasusi la mazingira lililo na makao yake mjini London.

Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo wa Uchina nchini tanzania mwaka ulioipita ambapo zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili kutokamatwa.

Pembe za ndovuShirika hilo pia linadai kwamba wajumbe waliokuwa wakiandamana na Rais Xi walinunua viwango vikubwa vya pembe hizo.

Uuzaji wa Pembe za ndovu ulipigwa marufuku mwaka 1989 ili kuwazuia wawindaji haramu kuwaua ndovu
Habari Na BBCswahili.com

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.