Kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Aendelea Vyema Sana na Matibabu Anayopatiwa Nchini Marekani
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi wa Tanzania nchini Marekani
Mhe Liberata Mulamula aliyekwenda kumjulia hali katika hospitali ya John
Hopkins iliyopo Baltimore, Maryland, nchini Marekani, leo Jumapili,
siku moja baada ya kufanyiwa upasuaji wa Tezi Dume.Picha na IKULU
Habari kutoka hospitalini hapo zinasema Rais Kikwete anaendelea vyema na leo asubuhi alianza mazoezi ya kutembea, kuashiria kwamba mambo yote ni mswano. Tutaendelea kwuashirikisha taarifa ya maendeleo yake mara kwa mara. Tuzidi kumuombea apate nafuu haraka ili arejee nyumbani
kulijenga Taifa
No comments: