Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways linasema limepata hasara ya dola milioni 116 katika kipindi cha nusu mwaka kinachomalizika mwezi huu wa Novemba.
Shirika hilo linasema hasara hiyo imetokana na mlipuko wa Ebola
katika nchi tatu za Afrika Magharibi na kuzorota kwa hali ya usalama.
Mwandishi
wa BBC aliyefuatilia taarifa hiyo Emmanuel Igunza anasema kuwa huu ni
mwaka wa pili kwa kampuni hiyo kurekodi hasara. Idadi ya wasafiri
imepungua mwaka huu kutokana na taarifa kuhusu hali mbaya ya usalama
nchini Kenya.
Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Mbuvi Ngunze anasema
utendaji wa shirika hilo pia uliathiriwa na kusitishwa kwa safari za
ndege katika mataifa ya Sierra Leone na Liberia -chi ambazo ziliathiriwa
zaidi na Ebola.
Katika kipindi cha kati kati ya mwawezi wa
Augost, Kenya Airways ilitangaza kuwa imesitisha safari zake katika nchi
hizo mbili Safari hizo bado hazijafufuliwa.
Ngunze ameonya kuwa mapato ya kampuni hiyo yanaweza kushuka hata zaidi kama shirika hilo litaendelea kusitisha safari hizo.
Lakini si kampuni hiyo tu iliyoathiriwa na mlipuko wa Ebola katika nchi za Liberia, Sierra Leone na Guniea.
Shirika
la ndege la Ethiopia, Ethiopian Airlines pia hivi karibuni lilisema
kuwa mapato yake yameshuka hadi kwa kiwango cha asilimia 20 kufuatia
hofu ya wasafiri juu ya Ebola.
No comments: