Suala la wapenzi wa jinsia moja na sheria nchini Uganda baado linazua mijadala nchini humo
Miezi mitatu tangu mahakama nchini humo kuibatilisha sheria dhidi ya
ushoga kwa sababu za kiufundi sasa habari zingine zimeanza kujitokeza
kuhusu uwezekano wa serikali kuleta tena muswada huo bungeni.
Kujitokeza
tena kwa suala hilo wakati huu ni baada ya hati maluum kuvujishwa .
Hati hiyo ya kurasa tano ni ya muswada jaribio kuhusu suala la mapenzi
ya watu wa jinsia moja.
Hati hiyo inaitwa : 'Mswada wa mwaka 2014 kuzuia kueneza visa vya kujamiiana ambavyo si asili wa mwaka wa 2014.
Katika
hati hiyo kuna pendekezo la kifungo cha miaka saba ikiwa mtu
atapatikana na hatia ya kile kinachoweza kuitwa kufagilia ushoga.
Neno lilotumiwa ni kutangaza na hivyo kutiliwa mkazo badala ya sheria ya zamani iliokuwa inatilia mkazo ushoga wenyewe.
Wachambuzi
wanasema kuwa hati hii ikipasishwa kama sheria itakuwa mbaya zaidi ya
ile iliobatilishwa kwani itawahukumu watu wengi mkiwemo vyombo vya
habari pamoja na watu wote wanaotumia mitandao yote ya kijamii
Hati hii inasema kuwa mtu yeyote akipatikana na hatia atahukumiwa kifungo cha miaka saba.
Sheria
iliobatilishwa na mahama mapema Agosti mwaka huu miongoni mwa mengine
ilikuwa inasema yeyote akipatikana na hatia atafungwa jela maisha.
Waziri
wa taifa wa sheria na naibu mwanasheria mkuu Fred Ruhindi akizungumza
na BBC kwa simu amekataa kutoa kauli kwa kile alichoita hati
iliovujishwa na kusema kuwa mchakato kuhusu sheria mpya ya kudhidbiti
ushoga unaendelea.
Yeye waziri anaehusika na maadili Padri Lokodo amesema hajui lolote kuhusu hati hiyo.
Punde baada mahakama kubatilisha sheria hiyo mapema mwezi Agosti
mwaka huu, chama tawala cha NRM kiliunda kamati maalum ya watu 10,
ikiongozwa na makamu wa rais Edward Sekandi, kutahmini muswada hatua
hiyo.
Hadi sasa haijatoa taarifa yoyote kuhusu kazi yao mpaka muda huu ambapo hati ya mwaswada kuvujishwa.
Mchakato wa kuunda sheria dhidi ya ushoga ilianza mwaka wa 2009 na imepitia awamu kadhaa kutokana na utata wa suala hilo.
Huku
wanaounga mkono kuweka sheria kali dhidi ya mapenzi hayo, baadhi ya
makundi ya kutetea haki za binadamu pamoja na mataifa ya magharibi
yanapinga hilo yakisem ani kugandamiza haki za bindamu.
Na
serikali pamoja na mashirika ya misaada ya kimaghari yamekata miaaada
kwa serikali ya Kampala kuhusiana na suala la mapenzi ya watu wa jinsia
moja.
Na hivyo suala la mapenzi hayo baado linavuma Uganda
Habari na BBCswahili.com
No comments: