Ads Top

WAZIRI BITEKO ATEMBELEA SOKO KUU LA DHAHABU GEITA


Aahidi kuongeza Madawati Manne kuboresha huduma
Na Antony Sollo Geita.
WAZIRI wa Madini Mheshimiwa Dotto Mashaka Biteko akiongozana na Ofisa Madini Mkoa wa Geita Bwana Daniel Mapunda leo julai 23 wametembelea Soko Kuu la Dhahabu lililopo katika Halmashauri ya Mji wa Geita na kujionea namna wadau wa Sekta ya Madini walivyoitikia wito wa Serikali wa kuwataka wadau kuuzia Madini katika Soko hilo ili kuiwezesha Serikali kupata taarifa za Mapato pamoja na kuwatambua wadau wa Sekta hiyo.
Baada ya kuwasili katika Soko hilo Waziri Biteko pamoja na Ofisa Madini walikuta umati mkubwa wa watu waliofurika katika viunga vya Soko hilo kwa ajili ya kupata vibali ili waweze kuuza Madini yao kwa njia ya halali ambapo Waziri Biteko aliwapongeza kwa namna walivyoitikia wito wa Serikali na kuwaahidi kuongeza Madawati (4) kwa ajili ya upimaji kwenye Soko Kuu ili waweze kuboresha huduma kwa wateja.
“Nimefurahishwa na namna mlivyojitokeza na kuitikia wito wa Serikali,niwaombe ndugu zangu  muwe wavumilivu wakati Serikali inafanya mchakato wa kuongeza Madawati (4) ambayo yatasaidia kuhudumiwa kwa haraka”alisema Biteko.
Kwa sasa Soko Kuu la Madini la Mkoa wa Geita lina dawati (1) linalohudumia wateja kati ya 30 hadi 80 kwa siku ambapo idadi hiyo imeongezeka kwa kasi jambo linalowapa usumbufu wateja na hilo ndilo limepelekea kumshawishi Waziri Biteko kuona kuwa kuna haja ya kuongeza Madawati manne ili kuboresha huduma.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Ofisi ya Madini Mkoa wa Geita,idadi ya wateja imeongezeka sana kwa kipindi cha kuanzia julai 20 mwaka huu ambapo kuanzia tarehe 20 hadi 23 julai mwaka huu wateja wameongezeka kufikia 280 kwa siku tofauti na kipindi cha nyuma ambapo kulikuwa na idadi ndogo ya wateja kati ya 30 hadi (70) kwa siku.
Ujio wa Waziri Biteko umeleta faraja kwa wadau wa Sekta ya Madini ambapo wamesema utaondoa kero za wadau wa Sekta hiyo na kwamba mwishoni mwa wiki hii wachimbaji wadogo waliliambia Tanzania Daima kuwa kuna changamoto ya Masoko na watumishi wanaowahudumia katika maeneo mbalimbali yanapopatikana Madini ya Dhahabu Mkoani Geita na kuiomba Serikali iongeze watumishi ili kuboresha huduma hiyo.

MWISHO


No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.