Ads Top

MAISHA & MAHUSIANO

 

NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE

Kila mwanamke aliye na hekima huijenga nyumba yake: Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’. Tafsiri ya neno nyumba ni familia, naam na familia inajumuisha baba, mama na watoto endapo mmejaliwa. Hata hivyo katika hali ya kawaida watoto watalelewa katika msingi mzuri endapo ndoa husika imetengamaa. Ifahamike kwamba hili andiko si la wanandoa peke yao, bali hata wanawake wasio wanandoa wenye familia kama wajane, walezi nk linawahusu. Kwa kuwa hapa tunazungumzia habari za wanandoa nitalifafanua zaidi kutoka kwenye kona hiyo. Pia neno nyumba limetumika ili kutupatia urahisi wa kuelewa namna nyumba za kawaida zinavyojengwa ili tueguze dhana hiyo kiroho pia. Kwa lugha rahisi ndoa yako ni nyumba, hivyo ubora, uzuri na mvuto wa ndoa yako unategemea namna unavyoijenga daima kwa hekima.
Ni vizuri ukafahamu kwamba suala la ujenzi/maboresho ya ndoa yako ni jukumu la kila siku ya kuishi kwa ndoa yenu mpaka kifo kiwatenganishe. Kila mmoja katika ndoa ni lazima ahakikishe anasimama kwenye nafasi yake na kufanya yale yampasayo ili kuifanya ndoa yake kuwa bora zaidi. Endapo hakutakuwa na jitihada za wanandoa katika kuimarisha ndoa yao, Shetani atatumia fursa hiyo kuivuruga ndoa husika. Kujenga kunakozungumziwa hapa ni kule kuhakikisha ndani ya ndoa kuna mahusiano na mawasiliano mazuri baina yenu ambayo yatafanikisha kutekelezwa kwa kusudi la Mungu.
Ukweli wa ajabu na wa pekee
Ni ajabu sana kuona kwamba jukumu la ujenzi wa ndoa/nyumba amepewa mwanamke. Hii haina maana mwanaume hahusiki, hapana, bali ki-nafasi jukumu la ujenzi wa nyumba/ndoa ni la kwako mama. Kumbuka nilikueleza kwamba nafasi hizi tano za Mwanamke katika ndoa zinafanya kazi kwa pamoja na kwa kutegemeana. Katika nafasi hii ya ujenzi unapaswa kuhakikisha unajenga ndoa yako ili kuzuia kila ufa/fursa ambayo Shetani anaweza kutumia kuvuruga ndoa yako. Kumbuka katika hali ya kawaida kujenga ni kuimarisha/kuweka mazingira bora juu ya kile unachokithamini ili kuzuia madhara yanayoweza kutokea. Naam nafasi hii inalenga kukusaidia uwe makini sana na kila kinachoweza kubomoa ndoa yake.
7
Suala la ujenzi wa ndoa ni endelevu kwa sababu siku zote adui anatafuta kubomoa ndoa yako. Ni lazima uwe makini kujua wapi ni mahali palipobomoka ambapo Shetani anapatumia sasa kuharibu ndoa yako au anaweza kutumia baadaye kuharibu ndoa yako, naam ukishajua kwa kutumia hekima, jenga ukuta imara ambao adui hawezi penya. Kama ndoa yako ina nyufa basi ni rahisi adui kupita kwenye hizo nyufa. Kumbuka hata  kama umemaliza kujenga kila kitu kwenye nyumba yako, bado kuna matengenezo ya mara kwa mara yanahitajika ili kuifanya nyumba yako kudumu katika hadhi inayostahili. 
Maeneo ya msingi katika kujenga ndoa yako
  • Utiifu kwa mumeo
Maandiko yanasisitiza sana wanawake kuwatii waume zao (Waefeso 5:22-24,                1 Petro 3:1). Mitume walindika maandiko haya ili kuwaonya wanawake kutokana na mienendo yao mbele za waume zao kitabia na hasa katika suala zima la utiifu. Bahati mbaya baadhi ya akina mama sio watiifu kwa waume zao na tena wengine wana dharau kubwa sana. Naam fahamu kwamba Mke si Mke bila Mume, na Mume si Mume bila Mke. Hata siku moja ndoa yako haiwezi kujengwa kwa kiburi au dharau kwa mumeo bali utakuwa unaumba jambo baya sana ndani ya mume wako.
Najua unaweza ukasema tabia za mume wangu ndiyo zinazifanya kumdharau, kumsema vibaya nk. Suala sio tabia zake, bali ni wewe kutumia hekima katika kukabiliana na tabia zisifofaa za mumeo kwa kuwa kumdharau ni kuendelea kubomoa na si kujenga, naam  ni kuendelea kuleta tatizo na sio kutatua tatizo. Umeshawahi kuwaza juu ya jambo hili kwamba, Mke anaagizwa kumtii mume wake kama vile kumtii Bwana. Imeandikwa katika Waefeso 5:22 ‘Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu’. Je ni kweli ndivyo unavyomtii Mumeo? Naam haijalishi mume wako yukoje usionyeshe dharau, mtiii tu, ni mume wako.
Mtume Petro anawaonya wanawake akisema ‘kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno’ (1Petro 3:1). Sijui kama wewe Msomaji unaona uzito uliopo kwenye mistari hii. Kwa lugha nyepesi utiifu wa mke kwa Mume utawafanya wengine kumwamini Yesu mnayemtumaini. Naam na upande wa pili, kukosa utiifu kwa mumeo kutawazuia wengine kumwamini Yesu, je unajua gharama ya kuwazuia wengine kumjua Kristo kwa sababu ya kukosa utiifu kwa mumeo (asomaye na afahamu siri hizi).
Wanaume kadhaa walioko kwenye ndoa wamekuwa wakiniambia kwenye suala la tabia hawajaona tofauti kati ya wanawake wasiokoka na waliokoka. Na kikubwa wanachosema ni kudharauliwa na wake zao. Hata kama katika hali ya kawaida mumeo anafanya mambo yanayopelekea wengine kumdharau wewe usifanye hivyo yeye ni kichwa chako
Fahamu kwamba daharau ni sumu mbaya kwenye ndoa yako yako mama, jizuie kabisa. Naam utiifu ni kila kitu kwa Mwanume, binafsi nimegundua wanachotafuta wanaume kwa wake zao bila kujali elimu zao, uchumi wao nk ni utiifu, naam kumdharau mumeo ni kubomoa nyumba yako ni kumruhusu Shetani kuharibu ndoa yako, ni kumuingiza mume wako fikra za wanawake wengine tofauti na wewe.
  • Kutunza siri za mume wako
Katika kuijenga nyumba yako ni lazima ujifunze kutunza, kuhifadhi na kuficha mapungufu ya mumeo kwa wengine. Naam hiyo ndiyo hekima. Baadhi ya akina mama   bila hata kujali wanaongea na nani, wamekuwa wakieleza mambo ya ndoa yao na siri za waume bila hata kujua athari yake. Naam kufanya hivyoni kubomoa na si kujenga. Unawajibika kmtii na kumtunzia mumeo siri zake licha ya mapungufu aliyo nayo na uzidi kumwomba Mungu kwamba aiponye ndoa yako.
2
Naam na hata kama ni muhimu uwaeleze kwa lengo la kujenga basi ni muhimu kuwe na mipaka ya nani unazungumza naye na nini unawaweleza maana si kila kitu wanapaswa kujua cha wewe na mumeo. Katika kulisistiza jambo hili Paulo anawagiza Tito akimweleza kwamba awatumie Wazee wa kike wenye mwenendo wa utakatifu ‘Ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao, na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe’ (Tito 2:3-4).
  •  Matumizi ya kinywa chako
Mara kadhaa nimewasikia wanawake walioolewa wakisema maneno yasiyofaa kwa waume zao. Najua wengine ni kutokana na hasira na wengine kutokana na mfululizo wa matukio yasiyofaa ya mumewe. Nimesikiia wanawake wakiwaaita waume zao wajinga, wapumbavu, na mengine ambayo nisinependa kuandika hapa. Ninachotaka ukijue ni hiki, imeandikwa Mtu atashiba kwa matunda ya kinywa chake.
Tambua kwamba mume wako naye ana nafasi zake kama mwanandoa kwako, na nafasi moja wapo ni kuwa kichwa cha mwanamke. Sasa kila baya unalotamka kwake maana yake unaliumba kwenye kichwa chako mwenyewe na hivyo tarajia mabaya na uharibifu kwenye ndoa yako. Najua utaniambia Patrick kuna mambo yanaudhi sana na hayavumiliki, na mimi nitakujibu ni kweli lakini namna ya kushughulika nayo ni wewe kutumia hekima kama mjenzi na kuiponya ndoa yako na si kumesema vibaya.
Fahamu pia kwamba katika ulimwengu wa roho kuna pepo ambao kazi yao ni kufuatilia maneno/mawazo mabaya ambayo mtu anayanena ili kuyaumba yatimie. Mfano ukiwa na wazo kwamba kwamba Mume wangu si mzuri uwe una uhakika kuna pepo watakuja juu yako na kuhakikisha siku zote wana kufanya umuone mume wako mbaya.
Je hujasoma Zaburi 36: 4 inasemaje ‘Huwaza maovu kitandani pake, hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii”. Naam tafsiri yake ni kwamba hali ya sasa ya mtu huyo ni matokeo ya mawazo yake, naam mwanandoa huyu amewaza na kunena mabaya juu ya mume wake, na kwa sababu hiyo ameiingiza ndoa yake kwenye mabaya. Naam ni lazima ujifunze kunena mananeo yenye kuijenga ndoa yako na si kubomoa, ndivyo na nafsi yako, fikra zako zitakapokiri hivyo, naam ndivyo na BWANA Mungu naye atahakikisha hayo yanakujia.
  •  Msamaha (kusameheana)
Ndoa nyingi leo zinashida kwa sababu ya wanandoa kushindwa kusameheana.  Ni kweli kwenye ndoa kuna mambo mengi ambayo katika hali ya kibinadamu yanaweza kukufanya ushindwe kusamehe, nami kama Mwalimu sina budi kukufundisha kile ambacho neno la Mungu limeelekeza. Kumbuka imeandikwa tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote… (Waebrania 12:14). Naam watu wote wa kwanza akiwa na mumeo, hatutegemei uwe na mahusainao mazuri na watu wa nje, wakati mume wako hutaki kumsamehe, utakuwa unajidanganya nafsi yako.
8
Hivyo bila kujali Mumeo amefanya kosa ganii hakuna namna ni lazima ujifunze kusamehe na kusahau. Hii ni kwa sababu kutokusamehe ni kumpa Ibilisi nafasi ya kuendelea kuwavuruga. Si hivyo bali usitegemee kwamba hata maombi yenu nyote wawili yatakuwa yanasikilizwa. Maana kwa kushindwa kwako kusamehe una haribu mahusiano na Mungu (Mathayo 6:14) na kwa mwanaume kwa kushindwa kwake kukaa kwa akili na wewe kama mke, maandiko yanasema maombi yake hayatasikilizwa. Je unategemea nini kitatokea kama hautakuwa tayari kumsamehe.
  •  Kujali mahitaji ya mwenzako (tendo la ndoa)
Paulo Mtume aliwaandikia hivi wanandoa wa Korinto ‘Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu’ (1Wakorinto 7:1-5).
Kimsingi andiko hili linalenga wanandoa wote wawili, bali kwa kuwa ujumbe huu ni maalum kwa wanawake nitaandika zaidi upande wa mwanamke. Biblia iko wazi kwamba kwa sababu ya zinaa (tendo la ndoa) kila mume awe na mke wake mwenyewe. Moja ya sababu muhimu za wewe kuolewa ni ili kumtosheleza mumeo kwa habari ya tendo la ndoa kama ilivyo na kwako pia.   
Kwa wanandoa wengi haja ya tendo la ndoa inatofautina, hata hivyo mara nyingi uhitaji wa tendo la ndoa kwa Mwanaume uko juu kuliko ilivyo kwa mwanamke. Hata hivyo kila mmoja ana – muhitaji mwenzake ili kutoshelezwa katika hitaji hili muhimu. Baadhi ya wanawake kwa kujua ukweli huu na tofauti hii ya uhitaji wa tendo la ndoa, kwa kutokufikiri athari zake kwa wenzi wao, kwao binafsi na ‘future’ yao huwanyima waume zao haki yao ya tendo la ndoa hasa pale wanapokuwa wametofautiana juu ya jambo fulani. Mbaya zaidi wapo akina mama ambao wakikasirika huwanyima waume zao haki hii ya msingi kwa muda mrefu kwa mfano mwezi mmoja, minne, hata zaidi ya mwaka na wanaishi nyumba moja na wengine wanalala kitanda kimoja.   
Mume wako akijua kwamba unatumia ugomvi/tofauti zenu au hata kwa makusudi kumnyima haki yake ya tendo la ndoa, na jambo hilo likawa endelevu uwe na uhakika taratibu unaanza kuharibu ndoa yako. Maana, Shetani ni mzuri sana wa kutumia nafasi ambazo wana wa Mungu wanampa. Ndani ya mume wako yataingia mawazo mabaya (Ezekieli 38:10) na kumweleza ‘je mbona kuna wanawake wengi, ni suala la kwenda kumaliza haja yako kwa mwanamke yoyote mwingine’. Wazo jingine pia litamwambia kwa nini huyu mwanamke akutese kiasi hiki, kwa nini usiwe na nyumba ndogo nk. Uwe na uhakika endapo mumeo ameokoka, hofu ya Mungu ndani yake ndiyo itakayomzuia kufanya mambo haya lakini ukimuuliza taratibu atakuambia mawazo haya hunijia mara kwa mara unaponinyima haki yangu ya tendo la ndoa.
6
Naam, hata kama hatafanya hayo, uwe na uhakika kwamba tayari kwenye ufahamu wake umeshapanda mbegu mbaya na itaendelea kukua endapo utaendelea na tabia yako ya kumnyima haki yake. Ndiyo, usishangae siku moja kukuta mumeo ametoka nje ya ndoa, usikimbilie kumlaumu Shetani, maana wewe ndiye ulifungua mlango na kumkaribisha. Nakumbuka mwanandoa mmoja (Mwanaume) alisema hizi ndoa za Kikristo zinatutesa sana wanaume, na zinawafanya hawa wanawake wajisahau sana, kwa kuwa wanajua Biblia imetuzia kuoa mke zaidi ya mmoja. Naam ilibidi nitumie muda mwingi kurejesha ufahamu wa huyu ndugu kwenye msingi wa ki-Mungu kwa kuwa nilijua tayari kuna wazo lilishaingia moyoni mwake na nilijua wapi linampeleka.
Nimeandika jambo hili kwa kirefu kwa sababu mara nyingi sehemu kubwa ya kesi za wanandoa inapofika kwenye suala la unyumba, wanawake ndio wanao – wanyima waume zao. Naam nakiri hata wanaume wapo lakini ni mara chache sio kama ilivyo kwa wanawake. Mwanamke sikia, kitendo cha Mungu kukupa huyo mume ni heshima ya pekee sana kwamba ni wa kwako pekee yako. Ukitaka kujua gharama yake waulize wanawake ambao wana ‘share’ mume namna inavyowagharimu kihisia, kifikra na kimaisha. Naam ni lazima ujifunze kujali na kutimiza mahitaji ya mwenzi wako vinginevyo unafungua mlango kwenye ufahamu wa mumeo na kumwambia angalia kule nje kuna wanawake wengine (Asomaye na afahamu).
Ukweli ni kwamba kuna sababu mbalimbali ambazo hupelekea wanawake kwenye ndoa kufanya hivyo, ila ushauri wangu ni kwamba, uamuzi wa namna hii (kumnyima tendo la ndoa mumeo) ni wa kuharibu na si kujenga. Hivyo haijalishi huyo baba kakukosea nini (labda ziwe issue za kiafya), suala la tendo la ndoa kwake ni muhimu sana na ni haki yake, kutokumpa haki yake ni kukaribisha Shetani kwenye ndoa yako. Naam ni vizuri mka-hakikisha kwamba tofauti zenu zote mna – zimaliza kabla hamjaingia kulala, itawasaidia sana.
Kuna maeneo ambayo ningeweza kuandika pia, lakini hayo matano hapo juu ni msingi wa mengine mengi. Kutokana na urefu wa nafasi hii ya Mwanamke kama Mjenzi nimelazimika kuigawanya mara mbili kwa hiyo katika sehemu ya tano nitamalizia kipande kilichobaki ambacho ndani yake nitaonyesha mwanamke anawezaje kupata hekima ya kumsaidia kuafanya haya na nitaweka baadhi ya mifano yenye kusaidia.

NJIA AMBAZO ZITAKUSAIDIA KUPATA MKE/MME ZIFUATILIE KWA UMAKINI

 
JITAMBUE   
Kwanza wewe kama mwanamke/mwanaume mwenyewe unatakiwa ujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi unayemhitaji katika maisha yako.
Wanawake/wanaume wengi hawajui wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewa na kuumizwa moyo bure.

SIFA ZA UMTAKAYE
Keti chini na kuorodhesha vigezo vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.  

TUMIA MACHO
Anza kumsaka huyo mwanaume kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kuridhika na mwili kusisimka.

JENGA MAZOEA NAYE
Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

HAKIKI SIFA ZAKE
Jipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha keti chini na anza kujumlisha alama za vigezo ulivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika uliyechagua amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizokosa unaweza kumsaidia kuzikamilisha pole pole mkiwa kwenye maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

WEKA MALENGO
Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda waifahamu.
Hata hivyo, wataalamu wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

USHIRIKI WA NDUGU/MARAFIKI
Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huachana kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana.

TENDO LA NDOA
Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu tendo la ndoa na kuamua kuwa pamoja huku wakizingatia suala la afya na uzazi salama.

NDOA
Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si vema ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

 
UVUMILIVU
Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidiana.

Kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake

wanawake wanajikuta wakikabiliwa na swali la, je, mwanaume huyu ananipenda kweli
Kuna wakati ambapo, wanawake wanajikuta wakikabiliwa na swali la, je, mwanaume huyu ananipenda kweli? Hii hutokea pale anapokutana na mwanaume ambaye, huenda amevutiwa naye. Pengine mwanaume naye anaweza kuonesha kuvutiwa na mwanamke huyo.

Kwa hiyo, mwanamke hujiuliza kama akubali ombi la mwanaume huyo na kukubali kuzungumza naye au kuanzisha naye uhusiano, kama mwanaume atakuwa amezungumza naye kuhusu jambo hilo. ni kweli kwamba, kuna ugumu kwa mwanamke kujua hasa ni kwa namna gani anaweza kujua kwamba, huyo mwanaume amempenda kweli au hapana.

Kuna vitu vingi ambavyo vinaweza kuwa ni dalili ya kumpenda mwanamke, lakini wakati huo huo vinaweza visiwe.

1. Hebu tuchukulie kwamba, mwanaume ameonesha kuwa na tabia tunazoziita nzuri. Labda amekumbuka kirahisi jina la mwanamke, ameonesha kuwa msikilizaji mzuri, ameonesha kuwa anajali kuhusu kinachosemwa na mwanamke, na amekuwa anamuuliza maswali kwa dhati na utulivu. Hapa mwanamke anaweza kuamini kwamba, huyu mwanaume anampenda. Lakini ukweli huenda ukawa ni kinyume chake. Inawezekana huyo mwanaume ni muungwana tu, na anaonesha tabia hizo kutokana na uungwana wake na siyo kutokana na kumpenda kimapenzi mwanamke.

2. Kuna watu ambao wana upendo, wamekomaa kihisia na wanajua kuhusiana vizuri na watu. Hii haina maana kwamba, kumwonesha mtu tabia hizo, kuna maana ya kumpenda au kumpenda sana mwanamke. Dalili hizi ni nzuri na inawezekana zikawa zinaonesha mwanaume kumpenda mwanamke, lakini mwanamke asilichukulie jambo hilo kwa namna hiyo.

3. Mwanaume anaweza kuonesha kuwa na udadisi kuhusu mwanamke kwa maana kwamba, kutaka kujua mambo yake, kumfuatilia au kuulizauliza kuhusu habari za mwanamke. Hii haina maana kwamba mwanaume amempenda kimapenzi. Inawezekana mwanaume akawa amevutiwa kimapenzi na mwanamke ndiyo maana akaonesha tabia hizo, lakini siyo lazima iwe hivyo. Kumbuka kwamba, mwanaume anaweza kuvutiwa na mazungumzo ya mwanamke, akavutiwa hata na namna alivyo usoni, hivyo akapenda kuzungumza naye lakini siyo kwa sababu anampenda.

4. Kuna wanaume ambao wana wake au wapenzi, lakini wanajisikia vizuri kusikiliza wanawake wengine au kujua tu habari za wanawake wengine, bila kuwa na haja ya kuanzisha uhusiano nao. Mwanaume anapompa mwanamke ‘ofa’ hasa ya chakula cha mchana au usiku, ni dalili ya wazi ya kuvutiwa naye. Hapa kuna uhakika mkubwa zaidi, labda tu kama mazungumzo yanayotajwa kufanywa wakati huo wa chakula yanafahamika, na ni ya shughuli maalum. Kwa hiyo ‘ofa’ ya chakula ni dalili nzuri na yenye uhakika. Lakini kuna jambo ambalo ni muhimu kwa mwanamke kulifahamu katika hali kama hii. Kuna wakati mwanaume kumpa ‘ofa’ mwanamke kwa chakula cha mchana au jioni, kunaweza kusiwe na maana ya moja kwa moja kwamba, uhusiano utaundwa. Inawezekana katika kutoka outing huko, mwanaume akaghairi. Kwa wengine huchukua muda hadi kuamua kuhusu kuunda uhusiano au hapana.

5. Hata mwanaume kuamua kumpeleka mwanamke kwa familia yao na kumtambulisha kama rafiki yake, ni hatua yenye kuonesha kwamba, mwanaume ameamua kumpenda mwanamke huyo. Lakini wakati mwingine hii inaweza ikawa ni janja yake kutaka tu kumthibitishia mwanamke ili amhadae vizuri, na wala hakuna maana ya uhusiano wa kudumu.

6. Kuzungumza kwa pamoja kuhusu masuala ya baadaye ya kiuhusiano, kama vile, idadi ya watoto na mambo mengine ambayo mara nyingi huzungumzwa na watu ambao tayari wako kwenye uhusiano ni dalili ya mwanaume kuvutiwa mwanamke. Lakini tatizo la jambo hili ni kwamba, kuzungumza masuala ya baadaye inaweza kuwa ni njia ya mwanaume kutaka kujisikia au kujua jinsi inavyokuwa katika mambo hayo. Inaweza kuwa pia ni njia yake ya kutaka kupima wanawake wanavyosema kuhusu masuala hayo. Lakini inaweza ikawa mwanaume huyo anatafuta kujua misimamo ya mwanamke huyo ili hatimaye afanye uamuzi. Kwa hiyo, bado haioneshi kuwa amevutiwa na kuamua tayari.

Mara nyingi wanawake hudanganywa na dalili fulani zinazooneshwa na wanaume wakati wanapoanza kuzoeana nao. Dalili hizi huwafanya kuamini kwamba, wanaume hao wamewapenda tayari, wakati siyo kweli. Kwa kuangalia baadhi ya dalili hizo kama nilivyozitaja, mwanamke anaweza kuwa makini wakati anapoanzisha uhusiano, ili asikurupuke na kujikuta amedanganyika. Ni kweli, kuna wakati ni dalili zinasema kweli, lakini kuna wakai zinadanganya kuhusu kupenda au kupendwa

FIDA YA UAMINIFU KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI
 · Kwa kuanzia, kuwa katika mahusiano ya kimapenzi kuna faida nyingi kwa mwili, watu walio katika mahusiano bora ya mapenzi huishimaisha marefu na kufurahia afya njema kuliko wale wasiokuwa katika mahusiano ya aina hiyo. Faida hii haina pingamizi kwa sababu ya ukweli kwamba watu wanaokuwa katika mahusiano ya karibu wanajijengea hisia na nguvu fulani ambayo huwasaidia kusaidiana na kujaliana wakati wa shida. Siyo tu kwamba watu walioko katika mahusiano ya aina hii wanaishi muda mrefu lakini pia ni kweli kwamba wanakuwa na furaha na wanaridhika na maisha kuliko wale wanaoshindwa kukaa katika mahusiano.
· Pili, kuwa katika mahusiano mazuri ya mapenzi kunasaidia katika mambo mbalimbali ya kimahitaji. Kusaidiana katika mahitaji mbalimbali baina ya wapenzi ni njia nzuri ya kuwa na maendeleo. Watu wawili wanaoshirikiana pamoja mara nyingi watakuwa na maisha mazuri zaidi ya yule anayefanya peke yake. Unapokuwa na mtu karibu wa kusaidiana naye katika mahitaji ni rahisi kupata mafanikio.
· Tatu, Watu walio katika mahusiano mazuri wanapata msaada wa kijamii; kwa maana ya kuwa na mtu karibu ambaye anajali mahitaji yako ya msingi na hisia zako. Kuwa na msaada wa aina hii kuna faida nyingi, mojawapo muhimu ni kuweza kufanya maamuzi ya busara bila kuwa na mtindio wa mawazo na hofu ama mashaka.
· Nne, kuwa na mwenza katika maisha hufanya maisha kuwa ya faraja zaidi. Kuwa na mtu ambaye mnaweza kushirikiana mambo madogo madogo ya maisha kama kuangalia Tv, kutembea, kula pamoja ni muhimu; inaboresha mahusiano na mara nyingi watu walio katika mahusiano ya aina hii wamekuwa na maisha bora zaidi.
· Tano, Mahusiano ni muhimu kwa sababu wapenzi wana kawaida ya kuangaliana tabia zao hasa zile ambazo ni haribifu, na wamekuwa na kawaida ya kuonyana ama kushauriana kuacha kufanya mambo mabaya na tabia mbaya. Kwa mfano watu walio katika mahusiano ya karibu wamekuwa na tabia ya kujaribu kuwashauri wapenzi wao kuacha kuvuta sigara, kupunguza pombe, kuacha kutumia madawa ya kulevya nk.
· Mwisho, Watu walio katika mahusiano bora ya kimapenzi wanafanya mapenzi mara nyingi zaidi kuliko wale walio pekee. Kufanya mapenzi mara kwa mara, kimpangilio ni muhimu kwa afya bora ya mwili na akili. *Ni muhimu kuzingatia kwamba kufanya huko mapenzi ambako ni bora kwa afya ya mwili siyo kubadilisha wanaume ama wanawake, ila ni kwa mwenza wako ama mke au mume na katika hali ya maelewano, uhuru na amani lakini pia kwa utaratibu unaostahili ndiyo upelekea kuleta faida hiyo.
Baada ya kusema yote hayo, ni ukweli kwamba mahusiano mazuri baina ya wapenzi huwa na faida nyingi kwa watu wenye bahati ya kupata mtu wa kumpenda na hatimaye nao kupendwa pia.

Umesha wahi kujiuliza Hivi anakutesa au unajitesa mwenyewe?

Wengi wamekuwa wakiumia sana mioyo yao kutokana na ama kukosa penzi la kweli au kuingia katika penzi la kitapeli wakiamini ni penzi la dhati. Tatizo hili limekuwa likiwasumbua wengi, inawezekana hata wewe unayesoma makala haya, limewahi kukukuta au upo katika tatizo hili hivi sasa.

Tatizo hili husababishwa na kukosa umakini ikiwa ni pamoja na kutofuata taratibu sahihi kabla na baada ya kuanzisha uhusiano wa mapenzi. Hapa sasa ndiyo chanzo cha matatizo. Wapendwa wasomaji wangu, unapokuwa na simanzi ni wazi kwamba kila kitu kitakuwa hakiendi sawa, maisha yanabadilika, kila unachokipanga kinavurugika, ufanisi wako kazini unashuka.

Siyo ajabu, bosi wako anafikiria kukufukuza kazi kutokana na kuboronga ofisini. Kimsingi simanzi ni tatizo sugu katika maisha ya kiuhusiano na ni vyema ikiwa umejifunza mapema jinsi ya kuepuka simanzi katika maisha yako ya kimapenzi.
Kuna mambo mengi ambayo wengi huyakwepa ama kwa kuyajua na wakati mwingine bila kujua kuwa wanakosea na mwisho wanajisababishia simanzi ya moyo.

Katika mada hii nitakupa dawa ya kukuondolea simanzi moyoni mwako. Inawezekana umeshakata tamaa, baada ya kuachwa na kila mwanaume unayeanzisha naye uhusiano ukiamini una mikosi, hapo utakuwa unakosea sana, huna balaa wala nuksi ndugu yangu, ni kutojipanga na kutokuwa na utayari wa kukutana na matatizo katika uhusiano.

Hata hivyo, kwa kupitia mada hii kwa makini utaingiza kitu kipya ubongoni mwako na kukufanya uwe mpya katika ulimwengu wa mapenzi.

Kuna wengine wamekuwa wakilia kila siku, inawezekana hata wewe unayesoma mada hii hivi sasa upo katika matatizo makubwa ya kimapenzi na huoni kama kuna sababu ya kuendelea kuishi.

Hapo unakosea sana ndugu yangu, maisha bado yanaendelea, unachotakiwa kufanya ni kujiweka tayari kukabiliana na matatizo yajayo, huku ukihakikisha kwamba huruhusu matatizo ya kujitakia katika maisha yako.

Vipo vipengele vingi sana ambavyo kwa kuvifuatilia kwa makini utaweza kuondoka katika utumwa wa mapenzi unaousumbua moyo wako na kuharibu taratibu za maisha yako.

KABLA HUJAANZISHA UHUSIANO
Kipengele hiki kinawahusu wale ambao bado hawajaingia katika uhusiano. Hapa nitafafanua mambo ya msingi ambayo unatakiwa kuzingatia kabla ya kuingia katika uhusiano utakaokusababishia matatizo. Hutakiwi kuwa chanzo cha matatizo rafiki yangu.

Hapa ni muhimu sana kwako wewe ambaye unatarajia kuingia katika uhusiano mpya. Umuhimu wake unatokana na ukweli kwamba, baada ya kugundua vitu vya kuepuka kabla ya kuingia katika uhusiano itakusaidia kufanya maamuzi sahihi na kuingia katika uhusiano mzuri, wenye mwanga mbele yako.

(i) Tafakari...
Simanzi huletwa na mateso ambayo mhusika huyapata akiwa katika uhusiano ambao hakuutarajia. Hii inamaanisha kwamba ama mpenzi uliyenaye hakupendi au wewe mwenyewe umegundua kwamba humpendi!
Hisia hizi zinatosha kabisa kukuingiza katika simanzi ya moyo. Kugundua kwamba mpenzi uliyenaye hakupendi kwa dhati ni tatizo kubwa sana, maana hapa lazima ataanza kukufanyia vitimbi na kukukosesha raha.

Kitendo cha kuanza kumfikiria au kuwaza juu ya mabaya anayokufanyia ni mwanzo wa wewe kufanya vibaya kazini, kutojijali, kupoteza hamu ya kula na mwisho hata afya yako itakuwa ya mashaka.

Katika kukabiliana na hili ni lazima ufikirie zaidi kabla ya kuingia katika uhusiano na patna mpya. Ukiondoa suala la yeye kukupenda, jiulize je, unampenda? Ni kweli moyo wako umeridhika naye?

Umempoteza na unataka kumrudisha mikononi mwako





Kugombana ni sehemu ya maisha ya binadamu. Yawezekana kabisa ulikuwa na mwenzi wako ambaye ulimpenda kwa moyo wako wote na sasa mmeachana. Kutengana kuna mambo mengi, wakati mwingine ilikuwa hasira tu.
Siku zote baada ya hasira kuisha, moyo hubaki peke yake katika nafasi yake halisi ya kufanya maamuzi. Hapo ndipo kwenye lengo la mada yetu ya leo. Kwamba kwa msingi huo umegundua kwamba kumbe mpenzi wako uliyeachana naye, bado unampenda.
Kwamba hata makosa aliyokuwa akiyafanya, ulimsababishia au si makubwa kiasi cha kuachana na badala yake mnaweza kukaaa na kuzungumza kiutu uzima na kuyamaliza. Yes! Hilo ndilo ninalotaka kulizungumzia.
Upo tayari rafiki? Je, uko katika kundi hilo? Unataka kumrudisha mpenzi wako wa zamani? Kama majibu ni ndiyo, mada hii inakuhusu sana.

JE, NI SAHIHI?
Baadhi ya watu huamini kwamba kurudi kwa mara nyingine kwa mpenzi wa zamani ni kujidhalilisha, kujishusha na kujisalimisha. Kwamba hakuna mwanaume wala mwanamke mwingine yeyote atakayeweza kuwa naye tofauti na huyo anayemrudia.
Jambo hilo si la kweli hata kidogo, kikubwa cha kuzingatia hapa ni moyo; je, unahisi bado unampenda? Ni kweli naye anakupenda? Kama sifa hizi zipo, hayo mambo madogo ambayo mmetofautiana ni ya kawaida kabisa ambayo mnaweza kurekebishana taratibu.
Kwa msingi huo basi, hakuna tatizo lolote katika kurudiana na mpenzi wako wa zamani, maana tayari unakuwa umeshamjua vya kutosha, hivyo kukupa urahisi wa kufanya yale anayoyapenda na kuepuka asiyopenda jambo litakalozidisha umri wa uhusiano wenu, si ajabu mkaingia kwenye ndoa.

UTAFAIDIKA NA NINI?
Utafiti usio rasmi nilioufanya, unaonesha kwamba zipo faida za kurudiana na mpenzi mliyeachana, lakini kikubwa ni awe moyoni mwako.
Hebu msikie Julius Kihesupe wa Uwanja wa Ndege, jijini Dar es Salaam, ambaye alipata kuzungumza nami hivi karibuni akitoa maoni yake kuhusu suala hili: “Si vibaya kurudiana, maana kwanza mnakomaza uhusiano.
“Kumrudia mtu wako wa zamani maana yake ni kwamba umekubaliana na udhaifu wake wote. Unajua anachopenda na anachochukia, hapo lazima mtadumu. Bila kudanganya, mke wangu wakati wa urafiki wetu, tukiwa na miaka miwili kwenye uhusiano tulitibuana tukaachana.
“Kila mmoja alikaa kivyake kwa miezi kama sita hivi, nikakutana naye Dar, nikiwa nimeachana naye Mbeya, nikamwita tukakaa na kuzungumza, miezi minne mbele yake tukafunga ndoa.”

CHUNGUZA ALIPO
Kitu cha kwanza kabisa ambacho unatakiwa kuchunguza ni mahali anapopatikana kwa wakati huo, nasema hivyo kwa sababu yawezekana alihama makazi, kikazi n.k. Kujua anapopatikana ni mwanzo wa kuelekea kwenye mafanikio ya kumkamata katika himaya yako.

ANA HISTORIA GANI?
Lazima ujue kuhusu historia yake kiuhusiano baada ya kuachana na wewe. Hapo unatakiwa kufanya ‘ushushushu’ wako kimyakimya bila yeye kujua. Ikiwa ameshafanya ‘vurugu’ sana, maana yake ni mtu asiye na msimamo na huenda anaongozwa zaidi na tamaa za kimwili na si mapenzi.
Katika kipengele hiki, ni muhimu sana kujua kama muda huo ambao wewe unahitaji kurudi tena mikononi mwake kama ana uhusiano mwingine. Kimsingi kama atakuwa ndani ya uhusiano, itakubidi uhairishe zoezi lako.
Unatakiwa kufanya hivyo kwa sababu kwanza, anaweza kukubali kuwa na wewe wakati akiwa bado hajaachana na mpenzi aliyenaye kwa muda huo, hivyo kuwa kama mwizi tu kwa mwenzako.
Kubwa zaidi ni kwamba, utakuwa katika mapenzi ya kushea, jambo ambalo si zuri kisaikolojia na hata kiafya.

Kumbuka kwamba, unaweza kuwa na mwenzi wako, mkapendana kwa dhati na mkadumu kwa muda mrefu, lakini kwa bahati mbaya mkaachana kwa sababu ambazo mnazifahamu wenyewe.
Katika muda mfupi ambao utakuwa umeachana naye, anaweza kufanya mambo ya ajabu sana. Pamoja na kwamba moyo wako unamhitaji, lakini anaweza kuwa tayari ameshapoteza sifa za kuwa na wewe. Katika hali hiyo, ni sahihi kurudiana naye? Bila shaka jibu hapa ni siyo sahihi.
Wiki iliyopita tulianza kuangalia kama ni sahihi kurudi kwa mwenzi huyo, faida utakazopata kwa kurudiana naye, kuchunguza sehemu anayopatikana na kufuatilia historia yake baada ya kutengana kwenu.
Enheee! Sasa twende kwenye vipengele vingine.



MAWASILIANO


Ukishachunguza mahali alipo na kuridhika na historia yake ya kimapenzi baada ya kuachana na wewe, sasa unatakiwa kutafuta mawasiliano yake. 
Kupata mawasiliano yake ni hatua ya kwanza, kitakachofuata baada ya hapo ni kujenga mawasiliano. Hapo sasa inategemea na namna mlivyoachana, lakini kama hamkuwa na ugomvi mkubwa sana, basi unaweza kumtumia meseji za kichokozi mara nyingi uwezavyo kwa siku.
Majibu yake ndiyo yatakayokupa mwanga wa kuendelea na kipengele kingine. Kikubwa hapa ni kutozungumzia kabisa mambo ya mapenzi, badala yake iwe ni kumjulia hali na utani wa hapa na pale.



MPE MWALIKO


Baada ya kutengeneza mawasiliano naye, sasa unatakiwa kumwalika katika shughuli mbalimbali za kifamilia na binafsi. Mathalani umepata mwaliko wa kwenda kwenye sherehe au hafla fupi ya usiku, omba kampani yake.
Kama mtu mzima atagundua kitu kilichopo moyoni mwako. Hata kama atakuwa mwenye moyo wenye kutu, kutoka naye mbele za watu, kutamfanya akumbuke enzi zenu mlipokuwa mkitoka pamoja, hivyo kufikiria kurudi tena kwako.
Ikiwa ataamua kukuambia kwamba anaona mrudiane litakuwa jambo zuri zaidi, maana atakuwa amekurahisishia, lakini akinyamaza, basi njia inayofuata hapa chini ni muafaka kwake.



MVUTE KARIBU YAKO


Sasa unatakiwa kumsogeza karibu zaidi na wewe. Lazima afahamu kwamba, kuna kitu fulani kipo ndani ya moyo wako. Meseji zako zibadilike, kama ulikuwa unamwandikia, “Vp uko poa?” au “Mambo yanaendaje?”, sasa unatakiwa kubadilisha hadi “Niambie sweetie, uko poa?”
Meseji za aina hiyo zitamfanya aone tofauti na inawezekana kabisa akagundua kwamba upo kwenye mawindo ya kumrudisha tena kwako. Katika hatua hii katu hutakiwi kufungua mdomo wako kumwambia kuwa unataka kurudiana naye na badala yake unatakiwa kuacha vitendo vizungumze vyenyewe.



OUTING

Kutokana na ukaribu wenu, kumwalika katika mtoko wa chakula cha mchana au usiku, haitakuwa vigumu kwake. Hiyo itakuwa njia nyingine ya kumfanya awe karibu yako zaidi.
Mkiwa katika mtoko huna haja ya kuzungumza chochote kuhusu uhusiano wenu, labda kama yeye ataanzisha mjadala huo. Ongelea mambo mengine ambayo ni maarufu zaidi labda katika duru za siasa, sanaa n.k lakini si mambo yanayohusu mapenzi kabisa.
Kama kichwani mwake alikuwa amekufanya kama rafiki yake wa kawaida, mtazamo utaanza kubadilika taratibu na kuanza kutamani kurudi tena mikononi mwako. Jaribu kufikiria, kama umetoka naye, akiamini labda unataka kumuomba msamaha na kurudiana naye, wewe unaanza stori za soka! 
Bila shaka atajiona kama mpumbavu kichwani, si ajabu akaamua kujifunga mwenyewe kwa kuomba urudi tena kwake.



JADILI PENZI LENU

Hatua hii ndiyo muhimu zaidi hapa; sasa unatakiwa kuanza kuzungumzia juu ya uhusiano wenu. Mwambie jinsi ulivyokuwa ukifurahishwa na mapenzi yenu. Msifie alivyokuwa anajua majukumu yake na kukuonesha mapenzi ya dhati.
Si vibaya kama utamweleza pia sababu ambazo unahisi zilisababisha wewe na yeye kuachana. Kwa kauli hizo utampa nafasi ya kuchambua/kumjua mwenye makosa na mahali pa kurekebisha.


KIRI MAKOSA YAKO

kiwa kuna mahali unaamini ulikwenda kinyume na yamkini ndiyo sababu kuu iliyosababisha muachane, kiri makosa yako mbele yake. Mweleze kwamba wewe ndiyo chanzo cha matatizo na huenda kama si kukosea, msingeachana.
Kujutia hasa kama uso wako utawakilisha vyema kilicho moyoni mwako, kutamfanya akuone muungwana ambaye unatambua ulipojikwaa na sasa unataka kurekebisha makosa yako. Hapo utakuwa na nafasi kubwa ya kumnasa kwa mara nyingine.


MWELEZE YAKO YA MOYONI

Sasa huna sababu ya kuendelea kujitesa, toa dukuduku lako. Mwambie moja kwa moja kilichopo moyoni mwako. Kwamba unahitaji nafasi nyingine kwake, maana umeshajua makosa yako.
Hii ni nafasi ambayo si rahisi kabisa kuchomoka. Itumie vilivyo. Sauti yako pekee itoshe kumaanisha kile kilichopo moyoni mwako. Lazima atakuelewa.
Kama utakuwa umefuata kwa makini vipengele vyote hapo juu, lazima urudi tena mikononi mwake. Kuna nini tena? Ameshakuwa wako huyo, ila kuwa makini usimpoteze tena.

AKIKATAA JE?
Pamoja na kufuata vipengele vyote hivyo, inawezekana akakataa. Kukataa kwake lazima kuna sababu nyingi. Mwingine anaweza kukuambia moja kwa moja sababu za kukataa kurudiana na wewe wakati mwingine anaweza asiseme chochote.
Huenda akakumbia kwamba tayari ana mtu wake, au hafikirii kurudi mikononi mwako; usihuzunike.
Ni bora sana huyu anayekuambia ukweli, kuliko kurudi halafu ukutane na mateso yale yale.Inawezekana labda hana mapenzi na wewe. Kama ndivyo, kuna sababu gani ya kujikomba? Kubaliana na ukweli, halafu subiri mwingine!
Sikia, subiri mwingine na siyo utafute, maana mwenzi wa kweli huja mwenyewe, hatafutwi!


Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili.


na mwandishi wetu Boaz Stev
Nikuombe msomaji wangu kwamba unaposoma makala haya, soma kwa mtindo wa katikati ya mstari (between the line). Kuna somo kubwa mno kwenye mada hii kwa sababu wengi wapo kwenye mateso makubwa ya kimapenzi kutokana na makosa yao wenyewe.
Ukisoma ujasiriamali, utaelekezwa kwamba mafanikio yako yatatokana pia na namna ulivyo na nidhamu katika fursa unazopata. Inawezekana ukawa na bahati kwenye maisha lakini utabaki kuwa si lolote endapo hutatumia nafasi zako vizuri.
Kama maisha, ndivyo yalivyo mapenzi. Hayatanyooka, wala hayatakaa vema upande wako ikiwa hutakuwa na heshima kwa fursa utakazopata. Si suala la ujana au kujipanga, muhimu kwako ni kuheshimu kile kilichopo jirani yako. Zingatia: Mapenzi ni changamoto nzito.
Ukichezea penzi lako leo kwa sababu unazozijua wewe, tambua kwamba halitakaa kwako daima. Kama yalivyo maisha kwamba yapo mfano wa kioo, ukiyachekea yanacheka, ukiyanunia nayo yananuna. Ndivyo na mapenzi yalivyo. Ukiyachezea, nayo yatakuchezea kweli.
Unapaswa kuyaheshimu. Heshima ya mapenzi ni kumtunuku mapenzi ya kweli huyo ambaye amekujia na mapenzi yake. Umethibitisha anakupenda kweli, sasa kinachokuwasha nini mpaka uunyanyase moyo wake? Fumba macho, mara nyingi bahati huwa haiji mara mbili.
Inawezekana mwenzi wako wa leo ndiye mwenye mapenzi ya kweli. Ila wewe unausimanga moyo wake kwa sababu hana fedha. Unakwenda kuabudu wenye uwezo. Fimbo ya mbali haiui nyoka, kwa hiyo unaweza kufanya lolote, naye hatakuwa na cha kufanya zaidi ya kumuachia machozi na sononeko.
Kuna watu hawajiulizi hili; huyo anayekuja kwako akitumia fedha kukuteka kwenye himaya yake, ameshatumia jeuri hiyo kwa wangapi? Endapo utaujua ukweli, utakuja kufahamu kwamba ni wengi aliwanasa kwa sababu alitanguliza fedha.
Weka akilini kwamba haji kwako kwa sababu anakupenda ila anayo jeuri kuwa hutapindua kutokana na fedha alizonazo. Sasa basi, unapomkubalia unamfanya aongeze kiburi. Kesho atatupa ndoano kwa mwingine na huo ndiyo utakuwa mwenendo.wake
Atakutamani kwa sababu ya muonekano wako, kwa hiyo kutokana na kiburi cha fedha alichonacho, kesho akimuona mwingine atakayemtamanisha, atatumia fedha zake kumnasa. Hii ina maana kuwa mkondo wako, watapita wengi. Mwisho kabisa, utabaini kwamba uliingia katika msafara wa mamba.
Atapita kwa wenye tamaa za fedha, nawe utakuja kuingia humohumo. Hii ndiyo sababu ya kusema utajikuta umeunga msafara wa mamba. Wewe utasema unajiheshimu lakini huyo uliyeangukia kwake, hachagui.
Popote kambi, baadae unapata jawabu kwamba umechangia mwanaume na machangudoa wengi wa mjini.
Tatizo siyo mvuto wako, wapo machangudoa wengi mjini na wanavutia kwelikweli. Kama kavutiwa na wewe na katumia ngawira kukunasa, inashindikana vipi kuvutiwa na machangudoa wengine, nao akatumia fedha kuwanasa? Tena wao si gharama, kwa maana ndiyo kazi yao.
Vilevile kwa mwanaume, atampuuza mtu anayempenda na kumvaa mwingine anayemuona anavutia zaidi. Wengi wamefanya hivyo bila kujua kwamba hao wanaovutia barabarani, asilimia kubwa ni magubegube. Unahitaji mwandani wa maisha yako, tuliza akili.
Sikukatazi kutupa ndoano, ila jaribu kufikiria mara mbili. Uliyenaye hakutoshelezi? Kumuacha mpenzi wa kweli na kujishughulisha na wengine ni sawa na mfano wa mtu aliyepoteza almasi, wakati alipokuwa ‘bize’ akitafuta mawe. Usilie kama wenzako, tuliza akili leo.
Kuna watu wanateseka leo. Wanadai wana mkosi. Eti, mapenzi yanawachapa bakora kwamba hawana bahati nayo. Kama na wewe upo kwenye kundi hili, fumba macho halafu ufikirie ulipotoka. Je, hukumuacha aliyekupenda kwa dhati? Hukuchezea moyo wa yule aliyekuwa anakujali?
Kama jibu ni ndiyo, basi hutakiwi kulia. Mapenzi yalivyo, kupata mwenye moyo mkunjufu katika kupenda ni bahati nasibu. Hivyo basi, kama ulimchezea, ni zamu yako kuteseka kwa maana uliyachezea mapenzi. Ulimpiga teke anayekupenda, sasa unahangaika na wasiokupenda. Wanakuinjoi tu.
Karibu sana kwa maoni.

MAUSIANO YA KIMAPENZI KWA VIJANA KATIKA UMRI 18 HADI 20 FAIDA NA MADHARA YAKE:
FAIDA ZAKE KWA MVULANA.
FAIDA ZAKE KWA MSICHANA. 
(a)     KUTAMBUWA HISIA ZENU.
(b)    KUTAMBUWA ANAPENDA NINI NA KWA WAKATI GANI?.
(c)     KUTAMBUWA KUJIESHIMU KWAKE AU KUTOKUJIESHIMU.
(d)    KUTAMBUWA UZAIFU WAKE UKOWAPI?.
(e)     KUTAMBUWA UPENDO WAKE UTEGEMEA NINI?. N.K          
HASARA ZAKE KWA MVULANA.
HASARA ZAKE KWA MSICHANA.
(a)     KUPENDA KUPITILIZA UWEZOWAKO WA KIAKILI.
(b)    KUPENDA KUPELEKWA KATIKA MAJUMBA YA STAREHE.
(c)     KUPENDA KUTOWA NGONO PALE UNAPOSHAWISHIWA.
(d)    KUPENDA PESA ISIOKUWA ALALI UNAPOSHAWISHIWA.
(e)     KUWA NA MATUMIZI YASIOKUWA NA ULAZIMA. N.K

KUTAMBUWA HISIA ZENU.
Unawezaji kumtambuwa Rafiki yako hisia yake kwa muda mfupi. Huweze juwa kwa hali ya kawaida hadi uwenae kwa ukaribu hasa kwa kuongea anakwaana au kwa njia ya mawasiliano ya simu pia huwezi tambuwa hadi uwenae kimausiano kwa muda mrefu kwa miezi au miaka ndipo ujuwe hisia yake kwako N.K.
                KUTAMBUWA ANAPENDA NINI NA KWA WAKATI GANI?.
Unaweza kumtambuwa Rafiki yako anapenda nini na kwa wakati gani?, Kwa hali yakawaida unaweza ukadhani anakupenda sana kumbe hakupendi, Anachotaka ni kukuchezea na kukuacha baada ya kukujuwa mwili wako na tabia yako, nikazi sana kutambuwa anapenda nini?, Endapo utajitaidi kutulia na kujifanya mshamba utapata kujuwa anapenda nini na kwa wakati gani?, Pia kuwa makini usije ingia katika Mausiano ya kimapenzi hutaweza kujuwa utakapo ingia katika mtego huo.
             KUTAMBUWA KUJIESHIMU KWAKE AU KUTOKUJIESHIMU.
  Unaweza kutambuwa kujieshimu kwa rafiki au kutokujieshimu endapo utakuwa makini kutambuwa Hasira yake na Furaha yake husababishwa na nini?, Ndipo utajuwa kujieshimu au kutokujieshimu, Pia unapaswa kuwa makini sana, anaweza kujiweka katika hali ambayo unapenda naukaona kuwa nisawa hanatatizo lolote, kumbeamejificha tambuwa kuwa maisha bora yanatokana na wewe na wala si yule wala watu wale. Kuwa makini katika marafiki ulionao pia usiwe una nyanya paa marafiki walio geuka kitabia katika mazingira mnayoishi pamoja kila mmoja awemakini katika elimu na kuandaa maisha.
  
                   KUTAMBUWA UZAIFU WAKE UKOWAPI?.
Unaweza kutambuwa uzaifu wake na kumrekebisha au kumpataarifa mtu mwenye busara na kumrekebisha muusika uzaifu wake, nivyema unapoona uzaifu wamwezako yoyote tuwe na umoja wa kurekebishana katika kila jambo pia usiwe na haraka ya kumzarau au kumchukia katika uzaifu wake si sawa unatakiwa kuwa makini sana usijikute unabeba lawama katika nafsi yako kuwa makini katika maisha yako yenye msimamo.

                           KUTAMBUWA UPENDO WAKE UNATEGEMEA NINI KWAKO?.
Unaweza kutambuwa Upendo wa mtu yoyote kuwa unategemea nini?, Kuwa makini kujua hili wengi huwa awajuwi kuwa walezi wao au walimu wao wenye upendo wadhati kwa vijana unategemea nini?, Juwa unategemea kuona maisha bora na mafanikio yenye nidhamu na uaminifu wahali na mali kwako, nakujitengenezea sifa nzuri katika masoma na hata katika jamii inayokuzunguuka wewe kama kijana kuwa mwenye kupenda mienendo mizuri kimaisha.

HASARA KWA MSICHANA NA MVULANA.

KUPENDA KUPITILIZA UWEZO WAKO WA KIAKILI.
Inawezekana pia Isiwezekane kama ifuatavyo, Inawezekana umependa kupitiliza siku laumu inawezekana ujuwi madhara yake ukajikuta umependa pasipo kujuwa kwa kupewa vitu ambavyo wewe wala wazazi hawana uwezo navyo lakini wakati wako bado na kujikuta unapotea kupitia kwa mtu baki usiemjuwa na kumpenda, kuwa makini sana nihatari kwa maisha yako. Isiwezekane wewe kupenda kupitiliza na kuwa ulizi na kinga kwako kwa maisha yako unayo yaandaa hapo baadae, namaanisha katika umri wenu hutokea wawili kupendana kabla ya wakati na kuonekana katika jamii vibaya unaweza usijali ukaona nikawaida lakini wajivunjia heshima yako kwanza katika mwili wako na hata Elimu yako na familia yako, haifai kuwa hivyo unawavunjia heshima walimu pia kwa kujiraisisha kwenu ni Hatari kwa Maisha ya kila moja.
                             KUPENDA KUPELEKWA KATIKA MAJUMBA YA STAREHE.
Kijana mwezangu si kila mtu ni mwema kwako, juwa hilo na likukae akilini sisemi usipende ofa pima ofa zenyewe zinakusaidiaje wewe kama kijana na wakati wa ofa hiyo imekuja, Kwa wakati gani na imekufikia kwa kipindi gani? Pia unapaswa kuwa mwenye malengo kama kijana unaesoma na unaetarajia kuwa baba au mama wakesho aliebora zaidi, Utakapo bebwa kama mzoga nakupelekwa katika starehe juwa kuwa unapoteza muda wako katika kuandaa kesho yako kwa maana umebebwa na lolote litakalo tokea kwako litakuwa nisahihi likikukuta huna msimamo na ujielewi bora kuepuka mapema, Ni hatari kwa Maisha yako.  

                         KUPENDA KUTOWA NGONO PALE UNAPOSHAWISHIWA.
Kijana mwezangu unaesoma kuwa makini sana na kuepuka kutowa ngono pale unaposhawishiwa kwa mtego kuwa wewe si rijali kwa mvulana au wewe si mkubwa bado mtoto kwa msichana, sikia usihofu juu ya hilo hata kama akikwambia utaumwa usipofanya tendo la ndoa yote niyauwongo, Lakini kizazi chetu sis ni wale waitwao maskerepa na matupa niwengi sana, ivihatujuwi tunatengeneza kizazi kilicho dhoofika kwa hapo baadae, au kukosa kabisa kizazi??. Kuwa makini usijifedheeshe wewe mwenyewe ukajajuta mwenyewe wengi wanajuta kukosa watoto na kupata fedhea kubwa katika familia yake ni hatari kwa maisha yako kuchezea kizazi chako.    



                            KUPENDA PESA ISIOKUWA YA ALALI PALE UNAPOSHAWISHIWA.
Kijana mwezangu kuwa makini katika kupenda pesa au zawadi yoyote ile isiyo ya alali inaweza kutengenenza neno ushawishi fulani usioujuwa kwa maana, ukufikiri pesa au zawadi inamaana gani?, ulichukuwa tu ndiyo wale wanaopenda kupewa zawadi hujikuta zinawafunga waowenyewe hukosa chakujitetea sisemi usipokee zawadi nina maana mtu usiemnjuwa huweza kukupa zawadi usioifanyia chochote kwa mazingira ya kutatanisha, usipokee acha lakini wengine usema simu, pesa, kupewa lifti ya gari mimi siachi, siku katazi nakuelimisha mwisho wake si mzuri ni mbaya sana kuwa makini ni Hatari kwa maisha yako kuwa makini sana.  

                          KUWA NA MATUMIZI YASIO KUWA NA ULAZIMA.
Kijana mwezangu usiwe na matumizi yasiokuwa na ulazima kama vile, kwenda Disco, kwenda Hotel ya kifahari, kutemeleana kipindi cha masomo au katikati ya juma na kutokupangilia Muda vizuri n.k, matumizi kama haya yasiokuwa na ulazima umsababisha kijana kujiingiza katika mambo yasiyo faa kama vile kujiingiza katika mausiano ya kimapenzi kabla ya wakati wake kwa wakiume hata wakike chanzo kupenda makubwa mapema kabla ya wakati ni hatari kwa Maisha yako achakabisa kama bado usitamani kuingia huko akufai kabisa Onyo Hatari kwa Maisha yako. 
Imeandikwa na, Boaz Stev, Itaendelea !.

UMUHIMU WA SHANGA KWA WAKUBWA TU.



Nilivyogundua umuhimu wa Ushanga kwa akina dada Katika mapenzi.
 
Haya Akina Dada,
Somo leo ni USHANGA. Kwanza Ushanga ni nini? Kwa kimombo, ni beads. Ukipita mitaa Kariakoo, utakuta kila rangi na design zinauzwa na akina mama wa kiMasai (Wanafanya Consultation pia). Zile ndogondogo kabisa siyo hizo kubwa za kuvaa kwenye nywele. Ni pambo muhimu mno kwenye mwili wa mwanamke. Hata kwa watoto wadogo, aliyevaa shanga, unajua ni msichana huyo
Sasa mimi nilijifanya nime’zungu’tika, na kuaacha kuzivaa. Hasa baada ya ushanga niliyovaa kukatika na kumwagika nikiwa kwenye daladala. Uhusiano na boy-friend wangu ilikuwa kwenye Plateau…..yaani flet. Huyo boy-friend mimi nilimpenda sana. Nikaenda kwa Aunti yangu Temeke na kumwelezea shida yangu na kumwaomba Ushauri.

Aunti akanipeleka chumbani kwake. Akaniambia nivue nguo. Nilisita kwanza, lakini alisisitiza nivue. Nikavua. Akatazama mwili wangu, akasema, kweli mwili wako bado nyororo, lakini umekosa kitu kimoja muhimu….USHANGA!

Nilipigwa Butwaa… Ushanga! Aunti alisema, ndio umekosa Ushanga. Alienda akafungua Sanduku Lake, akanipa wenye rangi ya light blue, njano, na red. Nikazivaa kiunoni Aunti akaanza kutabasamu, akaniambia, haya vaa sasa na nenda kwa boyfriend wako. Uone kama mambo ni tofauti.

Nililudi nyumbani, nikaoga na kuvaa nguo ya Outing. Nikapanda daladala na kwenda mjini. Nilikutana na boyfriend wangu Posta Mpya …tukaelekea kwenye disko. Tulikuwa tunacheza madensi, halafu blues, ya Boyz to Men ikaanza kupigwa. Wenye disko walipunguza taa. Mimi na boyfriend wangu tukakumbatiana na kuanza kucheza Blues. Miili yetu iligusana na akaanza kunipapasa taratibu kufuatana na beats za muziki. Nilifurahi sana. Akateremsha mikono yake kwenye kiuno changu. Alivyogusa ile shanga aliyonipa Aunti akawa kama mwili wake imekufa ganzi. Alisisimuka we! Akanishika kwa nguvu, niligundua kuwa uume wake uli kuwa ATTENTION!

Akaniuliza taratibu na kiupole , "Chiku mpenzi, umevaa nini?"
"Nikamjibu kwa aibu , " Nimevaa Ushanga mpenzi".
Akasema, “Mimi najua kuwa ni ushanga ila tangu tuwe na uhusiano huja wahi kuvaa" shanga
"Kweli, mpenzi. Aunti amenipa leo"
"Huyo aunti wako mjanja, anajua mambo"

Wimbo ulivyoisha tukaondoka kwenda nyumbani kwake. Siku hiyo sex ikawa nzuri kuliko siku zote ambazo nilikuwa naye. Alikuwa na furaha mno. Kesho yake kazini kwake, akawa anatabasamu mpaka wenzake wakamuuliza ‘Vipi’. Na mimi nilipanda daladala kwenda Kariakoo, nilinunua shanga nyingi za kila rangi. Baada ya hapo nilienda duka na kumnunulia Aunti Zawadi ya Khanga kama shukrani.
Niliporudi Temeke kwa Aunti, alipoona natabasamu tu alijua mambo ni OKAY!
Akina Dada, ni muhimu sana kuvaa shanga. Ninjia moja ya kumtia ashki mpenzio.

Karibuni sana kwa maswali na kwa ushauri zaidi 
Imeandariwa Na
Mr. Stev B.






TABIA  HAIBADILIKI  ISIPOKUWA  MWENYE  TABIA  HIYO ABADILI  TABIA  YAKE: 
KUENDEKEZA  NAFSI:
SEHEMU YA PILI.


Suzana alikubali kulala na James kuazia usiku ule, usiku ule James alikuwa na furaha sana maana, Suzana alikubali kulala nae, James alitamani masaa yaende harakaharaka, huku Suzana akiwa anaendelea kuandaa chakula cha usiku ule, James nae akiwa chumbani kwake akiendelea kuangalia T.V ukuakisikiliza Redio nyimbo mwororo zikiendelea kumwelimisha na kumburudisha moyo wake, yapata saa 1:00 usiku Suzana amemaliza kupika chakula na pia anaandaa chakula meza ya sebuleni, baada ya kuandaa chakula meza ya sebuleni alienda kuoga nakuvaa vazi zuri sana la usiku, Suzana akatoka kuelekea mezani sebuleni akapakuwa chakula saani mbili tofauti na kuelekea chumbani kwa James, akagonga mlango kwa  James, na James hakuchelewa akawai kufunguwa mlango, James “ Oh! Suzana karibu sana”, Suzana “Asante James”, James akapokea sahani za chakula na kuweka mezani kwake, James “pole kwa mapishi Suzana” Suzana “Asante sana James” Suzana “karibu tule chakula” James “Asante Dear Suzana”, James akawa amebadilika sura yake akajawa na sura ya mahaba huku akiwa anakula chakula kwa uvivu sana, Suzana akamuuliza “vipi James mbona hivi?”, James akajibu “hapana nahisi kushiba baada ya kukuona Dear Suzana”, Suzana “Mmmmmh! James siunaniona”, James weacha tu Suzana “Nakupenda nashindwa hata kula, maana mzuka wapanda washuka wapanda washuka sijui ni nini”?, Suzana “Oh! James utakuwa sawa kuwa mpole kula bwana kula ehh!”, James akapokea chakula alicholishwa na Suzana, wakaendelea kula wakamaliza na Suzana akachukuwa sahani ya James na kupeleka jikoni, kisha Suzana akarudi chumbani kwa James, Suzana akaingia chumbani kwa James akakaa kwenye kochi, wakati ameingia chumbani  kwa James, James alikuwa amekwenda Kuoga. James akatoka bafuni huku akiwa amevalia taulo fupi na hakuvaa chochote zaidi ya taulo, na kumkuta Suzana ameketi katika kochi huku akiwa amevalia kanga moja ndembendembe huku akiburudika na DVD ya mahaba na nyimbo mwororo, James alipokaribiana na meza yake ya chumbani alichukuwa chupa iliokuwa na kinywaji kiitwacho Amarula, na kukifunguwa kisha kumimina katika glasi na kumpelekea Suzana pale alipokuwa ameketi, Suzana “Asante James”, James “ karibu tena ndani ya Moyo wangu Suzana”, Suzana “Asante sana James”, Suzana “kinywaji kitamu sana nimaziwa mazito sana sijawahi kunywa umekipata wapi James” ?, James “nimenunuwa dukani kwa ajili yako je umekifuraia”?, Suzana “Ndiyo James nimekifuraia sana”,  James na Suzana wakaendelea kunywa na kuburudika kwa nyimbo na DVD, huku Suzana akimshika James Mkono na kumpapasa James hadi mabegani mwake, James nae akapagawa alivyokuwa anapapaswa kimahaba na Suzana akahisi kuchanganyikiwa, mwili wa James ukasisimka mno, na viungo vyake vikastuka damu ya James ikatembea kwa kasi ya ajabu, na njasho njembamba sana kuchomoza kichwani, James akamalizia kinywaji kilicho katika glasi yake, na Suzana nae akamaliza kinywaji chake na glasi zikawekwa mezani na mchezo ukaaza, James akamuuliza “Suzana wewe ni mpenzi wa timu gani?”, Suzana akasema “napenda Man.UTD” na  wewe je?,  James Ok! “ Mimi napenda Bacelona”,yapata saa 2:00 usiku huku James akiwa amemshikilia Suzana kiunoni, na baada ya maswali hayo alimbeba na kumpeleka Suzana kitandani, Suzana alitoa sauti ya kimahaba “Nini bwana James”?,  James akajibu “Sweat heart Suzana I love you”, Suzana “ILove you two baby James”, James akamweka kitandani akaaza kushika miguu ya Suzana mmoja baada ya mwingine akipapasa na kuibusu, uku Suzana akilalamika “Oh! Oh! Oh! James asante”,  
James akipapasa hadi mapajani  mwasuzana, huku Suzana akihisi raha isioyakifani, James akapanda hadi kufikia kwenye maungio ya miguu na kiwiliwili, Suzana akatoa sauti nyororo, “James ah ah! ah! ah! Hapo unafanya nini James”? James “namumunya chokoleti my Love”, Suzana akapiga “kelele uuuuuaaaaaaamamaaaaaaaaaaaaaaa! Raha isioyakifani oh oh oh! Asante James”,  James akapanda hadi katika kitovu cha Suzana na kupapasa matiti ya Suzana huku Suzana akipiga makelele sana ya raha na utamu anaompa James, huku James akikutanisha jinsia mbili tofauti ziendelee kucheza mchezo huo unaoendelea katika uwanja wataifa wamahaba, Suzana akaongeza kelele pale James alipoamuwa kulamba masikio ya Suzana, huku wale wawili wakiendelea kucheza mpira piga nikupige, Suzana alihishiwa nguvu maana uwanja ulitawaliwa na James kwa muda mrefu sana, Suzana akatowa machozi wakati wanapeana chakula adimu cha usiku, Suzana akasema James “raha raha baba wanitesa chenga wanila magoli wanifunga ah ah ah ah ah ah! Umeshika msikani  James nipeleke utakavyo”, Suzana aliendelea kutowa kelele za mahaba “kushoto twende kulia twende juu twende baba raha utamu raha utamu James”,  James akaona kelele huzidi akamnyonya mdomo kwa  dakika kumi, Suzana alirukaruka kitandani kwa raha na utamu anaoupata kutoka kwa James, yapata saa 8:00 Usiku tangu walipo azamahaba huku James akihondomola chakula cha usiku bila ya kukosea njia, James akamwambia “Suzana pole asante sana”, Suzana “Oh! James unayajuwa mahaba ya ndani bila shaka jinamizi la mahaba litakuwa limekuachia”, Suzana “Pia niseme asante kwa ulichonifanya umeukuna Moyo wangu James”,  James “usijali mimi pia Suzana nahisi jinamizi litakuwa limeachia mwili wangu”, Suzana “James tulale sasa japo kidogo maana kunapambazuka sasa hivi”, James “ni kweli Suzana tulale”,. Asubuhi namapema James aliamka na kuelekea bafuni kuoga, huku Suzana akiwa katika uchovu sana alikuwa amelala usingizi, James akamaliza kuoga na kutoka kuelekea chumbani kwake, alikuta Suzana amekwisha amka na kutowa mashuka na kutandika vizuri mashuka mengine na kupafanyia usafi chumbani kwa James, James alishangazwa na Suzana nawakati alijuwa asinge weza kuamka mapema nakufanya yale aliyo fanya, James alijipunzisha katika kochi la chumbani kwake huku akiwa anakunywa maji ya Kilimanjaro, Suzana alikuwa bafuni kwake akifuwa mashuka na baada ya kufua alioga kisha akavalia vazi zuri lenye urembo na kuelekea jikoni kuandaa chai ya maziwa maana yapata saa 1:30Asubuhi, James akawasha T.V nakuweka DVD ya mchezo wakuigiza uliokuwa unahusu Kuendekeza Nafsi, ulikuwa unamhusu James, maana alikuwa hajuwi kuzibiti nafsi yake ikiamuwa jambo hutamani kulitekeleza jambo hilo, wakati anaangalia DVD hiyo, Suzana aligonga mlango nakuingia na chupa ya chai ya maziwa huku akiwa amebeba sahani iliokuwa na chapati za kumimina alizotengeneza kwa ufundi nzuri, James akamfungulia mlango na kumpokea na kupeleka mezani, Suzana akamkaribisha James “James Karibu chai mpenzi”  James “Asante Honey”, Suzana na James wakaketi na kunywa chai huku wakiwa wanatizamana kwa aibu, James akamtania Suzana “vipi baada ya chai tuendelee kuhondomola”?, Suzana akajibu “mwezio naumwa sana na tumbo sijajuwa ni nini”?, James Oh! Suzana “Pole sana utapona mpenzi nilikuwa nakutania tu Suzana”, James na Suzana wakacheka kwa pamoja huku wakisukumana kimchezo, waliendelea kunywa chai na walipo maliza, Suzana aliondoa vyombo vya chai na kumuuliza James, “mchana utakula nini”?, James “hapana nitakula usiku nimeshiba sana”, Suzana akamwambia   James, “naomba kwenda kupumzika James”, James akamruhusu “sawa Suzana kapumzike pole dear wangu ”, Na Suzana akaenda kupumzika, pia James akaendelea kuangalia DVD na baada ya muda mfupi James akalala gafla. Nakaribisha Maoni yenu ni muhimu sana.
Imeandaliwa na
Mr. Boaz stev,

TABIA HAIBADILIKI ISIPOKUWA MWENYE TABIA HIYO ABADILI TABIA YAKE :

NA MWANDISHI WETU BOAZ STEVE
KUENDEKEZA NAFSI: Kulikuwa na Asubuhi, Mchana, na Usiku iliwekwa kwa kusudi, sababu ndivyo Muumba wa Mbingu na Nchi alivyopanga.
Kunakijana Mmoja aitwaye James Steven, anaishi Mbezi Mwisho ni mwenye uwezo katika familiya anayoishi na wazazi wake wote kijana huyo niwakipekee sana katika familia hiyo yuko peke yake pia anaishi na mjakazi yani mfanyakazi wa nyumbani, anaeitwa Suzana. James anapenda kusoma na starehe kwa sana, James alihitimu shule ya msingi mtendeni na akabahatika kuchanguliwa katika shule ya I lala secondary school na kwa sasa nikidato cha Pili pia kijana huyo kutokana na umbali washule kuleanako soma, huwa na dereva ambaye anampeleka shuleni kila siku na kumrudisha nyumbani, Kwa mara nyingi hakai na wazazi wake kwa maana wazazi husafiri mara kwa mara hasa kikazi zaidi ingawaje maendeleo ya mtoto wao nimazuri sana, James hutumia nafasi ya shule vizuri na nafasi ya Wikiend vizuri sana, huwa hupenda kwenda kwa rafiki zake hata kwenda kutembea fukwe za bahari James hupendezwa na maeneo yaliyo tulia sana kwa wakati huo anaoitaji hutuliza akili na mawazo kuwa mapya zaidi,. Siku moja ilikuwa jumamosi wiki fulani ndani ya mwaka huu aliamka asubuhi sana akaelekea chumba kinachoifadhi funguo za gari akatoka nje akawasha gari nakuondoka kwenda Msasani, bila kuaga wakati yuko njiani alipishana na warembo tofautitofauti akiwa anaelekea msasani alipita katika kituo kiitwacho Mkwanjuni wakati anakaribia alimwona Dada Mmoja kwa jina hakumfahamu alikuwa mrembo sana, James gafla butwaa ikamkamata huku matematamu yakimdondoka kinywani mwake akashindwa kuvumilia akaamuwa kuwasha taa yakuashiria kuingia kushoto mwakituo hicho akasimamisha gari akiwa anatafakari, akujuwa kilichotokea wala kitakacho tokea akashuka kutoka ndani ya gari lake na kuelekea upande aliosimama Dada Yule, James alimsalimu dada Habari yako, dada akaitikia ‘’nzuri’’, James Sorry sijuwiunaelekea wapi?, Dada akasema Msasani, James naweza kukupa lifti, Dada Powa kwani unagari, James Ndiyo, Dada Powa twende, Wakaelekea katika gari ya James wakaondoka kuelekea Msasani, walipokuwa njiani James akamuuliza Dada Sorry unaitwa nani? Dada Akajibu ‘’Dayana’’, Oh! Dayana unajina zuri sana, Dayana asante nawewe unaaitwa nani? Mimi naitwa James,Dayana akasema kwa mshangao Oh! Nice Name, James naeakajibu Thanks, James akauliza Msasani unaenda kufanyanini? Dayana Naenda kazini, James Kazini! Ni kazi gan? Dayana Oh! No hupaswi kujuwa unaniuliza maswali mengi kama ni lifti nishushe nipande basi niende, James Oh! Sorry sitakusumbua tena wakawa kimya kwa muda, Wakiwa njiani wanaenda Msasani walifika kituo kiitwacho Namanga Dayana akaomba James ampeleke Oyster bay, James hakukataa akampeleka, kabla yahatuwa chache Dayana kufika anakokwenda akaomba kushushwa eneo fulani, James akamshusha Dayana akasema Asante sana kwa ukarimu wako, James akujibu kitu alitikisa kichwa hukuakiangalia maumbile na sura ya Dayana akisema Hahahahahaya! Alipatwa na Butwaa hakuweza kuondoka hadi kuhakikisha Dayana anakokwenda ni wapi?, James akaona Dayana ameingia katika nyumba nzuri sana ambayo James hakujuwa ni kwao Dayana au ni kazini ilimlazimu asogee hadi alipoingia Dayana katika geti la rangi Nyeupe James alipoona Nyumba ile kwa ukaribu zaidi ikampasa kuondoka haraka lakini hakwenda tena Msasani aliamuwa kurudi Mbezi Mwisho nyumbani kwao, Alipofika alipokelewa na Suzana ambaye ni Mfanyakazi pale kwao James na Suzana akamuuliza ulikuwa umetoka bila ya kuaga si sawa James ningeulizwa nawazazi ingekuaje? James akajibu sorry Suzana nilikuwa kwa rafiki zangu, hatahivyo nilisahau simu ndiyo maana nilikuwa sipatikani wakati unaponipingia simu, James akaingia Ndani kwake akaketi katika kochi lake akitafakari kilicho tokea gafla akaamuwa awashe redio aweke nyimbo mwororo zakumfariji pia akawasha T.V akaamua aweke DVD ya Mapenzi huku akiwa ameketi katika kochi, Suzana akagonga mlango kwa James akaingia akamwandalia Juice na keki James hakumwangalia alibaki kuangalia T.V Suzana akatupa macho akaenda kuzima T.V James akawasha akamsihi Suzana akimwambia niache niangalie mambo yakisasa maana nateseka sana Suzana akamuuliza James unateseka na nini? James akasema nashindwa kujielewa, Mapenzi yametawala fahamu zangu pia Moyo wangu cha zaidi nafsi yangu yaumia sana kuhusu kupenda Suzana, Suzana akajibu sasa dawa ndiyo hiyo James mimi sijuwi labda unisaidie dawa maana nimefikiri itakuwa hii Suzani, Suzana sikia James usiwaze sana sahau fikiria Masomo tu. James akasema siwezi nahisi kunajinamizi hunishika nakuniongoza sijajuwa linamaana gani?, Suzana nakuomba leo ulale na mimi iliupate kuliona jinamizi hilo yamkini utanisaidia litakapo jitokeza, Suzana hapana James mimi Dada yako hatupaswikulala pamoja James, James akamsihi kama hutaki kunisaidia umeniuliza iliiwenje naomba utoke nje Suzana nataka kuoga, Powa James, wakati Suzana anatoka kijiko kikadondoka chini Suzana akainama kukiokota kijiko hicho wakati anainama James akamwangalia maana Suzana alikuwa amevalia kimini/nguofupi ambayoilipanda kupitiliza mapaja ya Suzana huku yakionekana wazi, James akapata shida kuona paja za Suzani na baada yakuokota kijiko Suzani alitoka akaenda kuandaa chakula cha mchana na usiku huku James aliingia bafuni kuoga akitafakari mapaja alioyaona kwa Suzana hupata mzuka wakuwa na Suzana kimapenzi ingawa, James hajawaikuingia katika mapenzi nimara ya kwanza anapata mihemko ya mwili wake na hushindwa kujizuia pia tamaa huja moja kwa moja hujikuta hupenda na kutaka kumshika msichana, James akamaliza kuoga huku Suzana akiendelea kuandaa chakula, Kama kawaida ya James akaendelea kuangalia DVD yamapenzi na kusikiliza Nyimbo laini/za taratibu huku akitafakari, Dayana alivyomrembo mwenye umbo zuri na upande wa pili akiona Suzana akimtamanisha kwa njinsi alivyomsafi na mrembo muda wote akiwa jikoni na akiwa anafua pia huwa ni msafi sana mwenye kunukia manukato mazuri sana James wakati akitafakari, Suzana aligonga mlango nakuingia akiwa katika vazi la mchana akimpelekea chakula James chumbani kwake akiwa anaweka mezani, nguo ya juu ya Suzana ilipanda juu na Shanga zake kuonekana, pia James akamshusha macho kuangalia Nguo ya chini alivalia kimini chepezi chenye kuonyesha maungo kama yale aliokuwa akiangalia kwa T.V akaishiwa nguvu gafla akalala, Suzana alipomkaribisha chakula alikuwa kama asikii, James chakula tayari hakujibu, James chakula James akasema njoo tule wote Suzana akakubali wakaketi kula chakula pamoja wakiwa chumbani kwa James, wakiwa wanakula James akaona DVD katika kasha la DVD kulikua na picha za watu wawili wakilishana akapenda kumlisha Suzana naye Suzana akapokea wakati wanaendelea kula James alipaliwa na chakula, Suzana akamgongagonga kifuani na mgongoni nakumwambia Pole kula taratibu James, wakiwa wanaendelea kula James alikuwa ametegesha picha vibaya ikadondoshwa na upepo, Suzana akaenda kuokota alipo inamatema James alihisi mwili wake kuwatofauti hakuwa na hamu ya kula tena alibaki kusema jinamizi jinamizi linaniumiza sana Suzana, akarudi mbio Suzana akamwangalia ili ajue nijinamizi gani hilo? James akiwa anapiga kelele kwa sauti ndogo nateseka na jinamizi la Mapenzi, huku Suzana akiwa amemshika palekitandani akimbembeleza James akamuomba Suzana asije akakataa atakacho mwambia halafu akikubali ndipo jinamizi litapunguza nguvu yakumkaba na kumtesa basi, Suzana ilimlazimu akubali kwa chochote atakacho ambiwa na James,. James alimwambia Suzana naomba tulalewote ilinisijekupata matatizo usiku, Suzana alikubali kulala na James kuazia usiku ule Je kitatokea nini katika usiku huo wamanane? Kuwa makini kitakacho fuata nakaribisha Maoni yenu.
Itaendelea wiki jayo
UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.