Ads Top

SUALA LA AJIRA LAWA KIZUNGUMKUTI

KWA KILE  KILICHOZUNGUMZWA  KUWA  HALI MPYA,NGUVU  MPYA  NA KASI  MPYA  CHAJIDHIHIRISHA  HIVI  KARIBUNI NA BADO  KINAENDELEA KUJIDHIHIRISHA



NA;  mwandishi wetu Mbwana Ramadhania(anaripoti zaidi)
Kutokana na soko la ajira kuwa gumu na hali hiyo hadi kupelekea watu wa jinsia ya kike yaani wanawake wameonekana wakijihusisha na kazi ya  ukonda wa magari ya abiria aina ya dala dala na mengineyo yakiwemo  magari aina ya DCM  kwa  barabara  ya magari  ambapo hapo awali watu wa jinsia hiyo hawakuonekana wakijihusisha na  kazi hiyo
Aidha ;Wanawake wengi  hivi sasa wameonekana  wakipeana changamoto wao kwa  wao kupitia kazi hiyo kwani hivi jana mida ya asubuhi walionekana  wasichana  wawili wakiwa  wanaitia abiria na kupelekea kitendo hicho kuwa changamoto kwa wanawake wenzao ambao walikuwa wakipita pembeni  na wengine wakiwa  wamelipanda hilo gari
Aidha ;mwanaripota  wetu mwengine  kwa  jina aitwaye  Mohamedi  A. Nyamka  aliweza kuonana ana kwa  ana na miongoni  mwa makonda hao wa jinsia ya kike sehemu za Mbagala Rangi tatu  hivyo maongezi yao yalikuwa kama yafuatayo;
Mohamedi  Nyamka (mwandishi);habari  za saa hizi dada!
Kondakta(msichana);safi tu kaka
 Mohamedi  Nyamka (mwandishi)  ;Hivi kwanini  sasa hivi ninaona wanawake walio wengi wanajihusisha na ukondakta  ukitofautisha na hapo awali?
Kondakta(msichana)  ; Aaah! Ujue kaka  siku  hizi hali ya maisha imebadilika na sisi tumeona ni vyema tubadilike kwani wanawake walio wengi wanaona  ukondakta na kazi ya wanaume pekee kumbe la hasha hilo si kweli na sisi pia utegemezi uliokithiri kwa wanaume tunaona kuwa wanaume wenyewe wametuchoka na ndio maana tumeona ni vyema  tujihusishe na  kazi hizi, pia ninapenda kuwasihi wanawake wenzangu kuwa hii ni ari mpya na kasi mpya hivyo basi tujishughulishe tuache utegemezi kwa wanaume zetu kwani kazi ya ukondakta hata sisi tunaweza hususani kama mimi nilipata tabu hapo awali tu na tangia hapo hadi sasa nimezoea ninajionea kawaida tu kwani mwanzo mgumuuu!!!
Aidha ;mwanaripota  huyo  Mohamedi  A. Nyamka  hakuishia hapo aliendelea  kwa kuwapa  ushauri wanawake wengine kuwa  wasione ajabu kazi ya ukondakta kwa mwanamke kwani nayo ni ajira kama ajira nyinginezo  hivyo alimalizia kwa kusema  tunapomuelimisha mwanamke nisawa na kuwa  tumeielimisha jamii


No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.