Ads Top

IVORY COST YAIBUKA NA USHINDI ZIDI YA TOGO KATIKA MISHUANO YA KUWANIA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA


Didier Drogba akiwa na mashabiki wa Ivory Coast

Ivory Coast imeanza kampeini yake ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika kwa kuilaza Togo kwa magoli mawili kwa moja katika mechi yao ya ufunguzi ya Kundi D.
Ivory Coast ilipata bao lake la kwanza kunako dakika ya nane kupitia kwa mchezaji Yaya Toure na kwa mara nyingine, wachezaji hao wa Ivory Coast wanatafuta fursa ya kutwaa kombe hilo ambalo liliwaponyoka mwaka uliopita.
Nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba, analiongoza tena timu hiyo, kwa fainali hizo ambazo ndizo za mwisho atakazoshiriki.
Licha ya wengi kuipa timu hiyo ya Ivory Coast nafasi kubwa ya kushinda mashindano ya mwaka huu, The Elephants hawakucheza mechi ya kusisimua katika kipindi cha kwanza.
Mara ya Mwisho Ivory Coast, ilishinda kombe hilo ni mwaka wa 1992.

Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia bao lao

Togo nayo inaongozwa na mshambulizi wa Tottenham, Emmanuel Adebayor.
Dakika ya 44, Yahya Toure, nusura afunge bao la pili, lakini mkwaju wake uligonga mlingoti.
Ushirikiano kati ya Didier Drogba, Yahya Toure and Gervinho umeonekana kuwa nguzo ya timu hiyo ya Ivory Coast.
Dakika moja baadaye Togo ikasawazisha baada ya walinda lango wa Ivory Coast kufanya masihara, kwenye eneo la hatari.
Kufikia wakati wa mapumziko timu hizo mbili zilikuwa zikitoshana na nguvu ya kufungana bao moja kwa moja.
Lakini katika kipindi cha pili, Ivory Coast iliimarisha mashambulizi yake na kunako dakika ya 87, ivory coast ikapata bao lake la pili kupitia kwa mchezaji Gervinho.
Ivory Coast sasa inaongoza kundi hilo la alama tatu huku Togo ikiwa bila alama yoyote.
Kinyume na ilivyotarajiwa, mechi hiyo iligeuka na kuwa maonyesho ya nguvu, baina ya wachezaji kadhaa wanaoshiriki katika ligi mbali mbali za kulipwa na mara nyingi ilikuwa kati ya Kolo Toure na Adebayor na Vincent Bossou na Didier Drogba ambao walifanya makosa mengi na hivyo kuhujumu mtiririko wa mechi hiyo.
Mechi ya pili ya kundi hilo kati ya Tunisia na Algeria itaanza mwendo wa saa tatu za usiku majira ya Afrika Mashariki
.
Kikosi cha Ivory Coast Kikosi cha Togo
01 Boubacar Copa
04 K Toure
17 Tiene
21 Eboue
22 Bamba
05 Zokora
13 Konan
15 Gradel
19 Y Toure
10 Gervinho
11 Drogba

Wachezaji wa ziada

16 Yeboah
23 Sangare
03 Boka
14 Ismael
Traore
20 Lolo
06 Romaric
07 Razak
09 Tiote
02 Kone
08 Kalou
12 Wilfred
18 Traore
16 Agassa
02 Nibombe
05 Akakpo
06 Mamah
21 Dakonam Djene
08 Amewou
15 Romao
19 Kodjo Ametepe
04 Adebayor
11 Ayite
17 Gakpe

Wachezaji wa Ziada

01 Atsu
23 Tchagouni
09 Vincent Bossou
13 Sadat Ouro-Akoriko
20 Kokou
03 Dove Wome
07 Salifou
10 Ayite
12 Sapol Mani
14 Segbefia
18 Fessou
22 Damessi

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.