Jeshi la Marekani limeanza kuwapeleka nchini Mali kwa ndege wanajeshi wa Ufaransa pamoja na vifaa katika operesheni inayoendelea dhidi ya wanamgambo wa kiisilamu
Ndege tano za Marekani tayari zimewasili mjini
Bamako, huku ndege zengine zikitarajiwa kutua huko katika siku zijazo,
kwa mujibu wa msemaji wa jeshi hilo.
Ufaransa ilianza harakati zake dhidi ya
wapiganaji hao wiki mbili zilizopita kwa lengo la kuwakomesha wapiganaji
hao kuweza kuelekea Kusini mwa nchi.
Inajiandaa kuwakabidhi wanajeshi wa Kusini mwa
Afrika hatamu za kuendelea na harakati hizo. Kikosi hicho ni cha
wanajeshi 1,000 ardhini.
Takriban wanajeshi 2,000 wa Ufaransa kwa sasa wako nchini Mali huku kikosi kingine cha wanajeshi 500 wakitarajiwa kuwasili.
Kwa mujibu wa kamanda wa majeshi ya Marekani
barani Afrika, ndege za kuwasafirisha wanajeshi zilianza kuondoka kutoka
kambi ya jeshi Istres, Kusini mwa Ufaransa siku ya Jumanne.
Msemaji katika makao makuu ya jeshi nchini Marekani, aliambia shirika la habari la Reuters kuwa ndege tano tayari zimeondoka Ufaransa.
''Lengo letu ni kubeba, vifaa vizito kama magari
ya kivita , kulingana na jeshi la Ufaransa.'' alisema msemaji wa jeshi
Thierry Burkhard.
Uingereza, Belgium, Canada, Denmark na Italia
pia watatoa ndege za usafiri kwa kusaidia harakati za Ufaransa dhidi ya
wapigananaji.
Awali, Marekani ilisema kuwa itatoa msaada wa mawasiliano kwa wanajeshi hao.
No comments: