Ads Top

Jeshi la Marekani limeanza kuwapeleka nchini Mali kwa ndege wanajeshi wa Ufaransa pamoja na vifaa katika operesheni inayoendelea dhidi ya wanamgambo wa kiisilamu


Mwanajeshi wa Ufaransa akiwa kwenye harakati za kukabiliana na wapiganaji wa kiisilamu Mali

Ndege tano za Marekani tayari zimewasili mjini Bamako, huku ndege zengine zikitarajiwa kutua huko katika siku zijazo, kwa mujibu wa msemaji wa jeshi hilo.
Ufaransa ilianza harakati zake dhidi ya wapiganaji hao wiki mbili zilizopita kwa lengo la kuwakomesha wapiganaji hao kuweza kuelekea Kusini mwa nchi.
Inajiandaa kuwakabidhi wanajeshi wa Kusini mwa Afrika hatamu za kuendelea na harakati hizo. Kikosi hicho ni cha wanajeshi 1,000 ardhini.
Takriban wanajeshi 2,000 wa Ufaransa kwa sasa wako nchini Mali huku kikosi kingine cha wanajeshi 500 wakitarajiwa kuwasili.
Kwa mujibu wa kamanda wa majeshi ya Marekani barani Afrika, ndege za kuwasafirisha wanajeshi zilianza kuondoka kutoka kambi ya jeshi Istres, Kusini mwa Ufaransa siku ya Jumanne.

Msemaji katika makao makuu ya jeshi nchini Marekani, aliambia shirika la habari la Reuters kuwa ndege tano tayari zimeondoka Ufaransa.

''Lengo letu ni kubeba, vifaa vizito kama magari ya kivita , kulingana na jeshi la Ufaransa.'' alisema msemaji wa jeshi Thierry Burkhard.
Uingereza, Belgium, Canada, Denmark na Italia pia watatoa ndege za usafiri kwa kusaidia harakati za Ufaransa dhidi ya wapigananaji.
Awali, Marekani ilisema kuwa itatoa msaada wa mawasiliano kwa wanajeshi hao.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.