Ads Top

Chenga: Miaka 34 ya kuishi na nyoka

  
 
Bagamoyo. Ni mnyama hatari, mwenye sumu kali, anaogopwa, anaua, anaweza hata kukuachia ulemavu.
Hata hivyo Nobert Joseph Chenga, ameweza kucheza na kuishi na nyoka kwa miaka 34 sasa.
Siku hii, namkuta Chenga, maeneo ya Bagamoyo, akiwa katika moja ya kazi zake za kusaka na kufuga nyoka.
Alikuwa mchovu kwa sababu ya shughuli nzito ya kukamata nyoka kutoka mapori ya Miono, wilayani Bagamoyo.
Nilishuhudia nyoka wa aina mbalimbali wenye sumu wakiletwa katika mifuko maalumu.
Chenga mwenyewe ameshika fimbo maalumu ya kuwasogeza au kukamata nyoka.
Wanapofika, Chenga anafungua mkoba kwa ustadi kisha kuwaweka katika chumba, akitumia fimbo hiyo kuwasogeza mahali panapohitajika kukaa.
Wakati mwingine anawashika, kwa mikono lakini kwa namna ambayo nyoka hao hawawezi kuuma. Anawapanga katika vyumba alivyovipa majina kwa mfano; Black Mamba, Boom Slag. Green Mamba, Cobra, Msanga na African Venom.
Nyoka mmoja mweusi, niliyeambiwa anaitwa Black Mamba, akiwa na urefu wa zaidi ya futi tano, anaponyoka mikononi mwa Chenga, tukio lililonifanya nitimue mbio. Si mimi tu niliyetimua mbio, bali hata wasaidizi wa Chenga waliokuwa eneo hilo walikimbia. Hii ni kutokana na Chenga kuthibitisha kuwa nyoka huyo akikuuma, huchukui dakika tano, kabla ya kubadili jina na kuitwa marehemu.
Ananionyesha alama kadhaa za kuumwa na nyoka, mikononi na miguuni mwake. Lakini bado anaishi nao, anawafuga na anaendelea kuwakamata ili wawe wengi zaidi.
Mapenzi na nyoka yalianza 1979
Chenga alianza kupenda nyoka mwaka 1979. Mapenzi hayo kwa nyoka, hayakuja hivihivi, bali yalimwingia baada ya kupewa zawadi ya chatu mwenye kilo 60, akiwa mkoani Mwanza.
kwa habari zaidi bofya hapa..>>>> 

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.