Mtwara. Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini (CCM), Hasnein Murji jana aliachiwa baada ya kutimiza masharti yaliyotolewa na mahakama
            
Mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnein Murji (kushoto) akiingia katika 
chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mtwara  kusomewa shtaka la 
kufanya uchochezi. Picha na Haika Kimaro.  
Mbunge huyo alirudishwa rumande juzi kutokana na 
kushindwa kutimiza masharti. Sharti hilo lilikuwa ni kuwa na hati ya 
kusafiria ambayo aliiacha Dar es Salaam.
                
              
Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Mtwara, Dynes Lyimo 
alimwachia mbunge huyo kwa dhamana na hivyo kumtaka mtuhumiwa na 
mdhamini wake kusaini hati za kumtolea dhamana.
                
              
Baada ya maelezo yote, hakimu Lyimo aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 4,mwaka huu mahakamani hapo.
                
              
Mbunge huyo alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu 
Mkazi mkoani hapa mwishoni mwa wiki akituhumiwa kwa kosa la uchochezi 
anaodaiwa kuufanya Januari 19, mwaka huu eneo la Ligula mkoani hapa.
                
              
Hata hivyo viongozi wengine wa vyama vya siasa vya
 upinzani wanaohusishwa na vurugu za gesi wanatarajiwa kufikishwa 
mahakamani kwa mara nyingine kesho kusikiliza kesi inayowakabili yenye 
makosa matatu.
                
              
Viongozi hao ni Katani Ahmed Katani (33) na Said 
Kulaga (45) wa CUF, Hassan Uledi (35) wa NCCR Mageuzi na Hamza Licheta 
(51) wa TLP, wote wakazi wa Mtwara.
                
              
Mbunge huyo pamoja na wenzake hao wanashtakiwa kwa
 makosa ya uchochezi yaliyopelekea kufanyika kwa vurugu na kusababisha 
uvunjivu wa amani na mali za watu pamoja na miundombinu kuharibiwa 
vibaya.

  Tanzanian Shilling Converter
No comments: