Ads Top

Hisia kali zimezuka nchini Uganda kufuatia hatua ya Bunge la nchi kupitisha mswada unaonuia kuharamisha maandamano ya umma


Wakosoaji wanasema kuwa huu ni ukandamizaji wa haki na uhuru wa watu kukongamana

Watetezi wa mswada huu wanasema unanuia kuleta uthabiti, huku wakosoaji wakisema ni njama ya serikali kuzima upinzani.

Shirika la Amnesty International limesema kuwa mswada huo ni hatari sana kwa uhuru wa watu kuandamana nchini humo.

Mswada huo ulipitishwa licha ya kukosolewa sana na makundi ya kidini , wabunge wa upinzani na umma kwa ujumla pamoja na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Kuanzia sasa polisi watahitajika kutoa idhini kwa hata watu watatu wanaokusanyika katika sehemu za umma kujadili maswala ya kisiasa. 

Wanaouunga mkono mswaada huo wanasisitiza kuwa hauna nia mbaya ndani yake bali unaweza kutekelezwa.
Shirika la Amnesty linasema kuwa mswada huo ni sehemu ya ukandamizaji na hata ishara yake ikiwa kufungwa magazeti mawili na vituo viwili ya redio mnamo mwezi Mei mwaka huu kwa kuripoti madai ya njama ya serikali kutaka kuwaua wanasiasa wa upinzani.

Mswada huo ulipendekezwa mwaka 2009 na hatimaye kupitishwa kufuatia miezi kadhaa ya mijadala mikali nje na ndani ya bunge.
Ilipitishwa na bunge ambalo wabunge wengi wa chama cha rais Yoweri Museveni (NRM), licha ya upinzani mkali ndani ya bunge.

Mswada huo unawapa polisi nguvu za kuhoji mikutano yoyote ya hata watu watatu katika maeneo ya umma ya watu wanaojadili mambo ya kisiasa.

Polisi pia watakuwa na uwezo wa kuvunja mikutano ya zaidi ya watu watatu wanajadili maswala ya kisiasa majumbani kwao.

Polisi lazima wapokee maombi ya watu wanaotaka kukutana siku saba kabla ya kuwapa idhini na mikutnao inaweza tu kufanyika kati ya saa sita mchana na saa sita jioni

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.