Ads Top

SAKATA LA TOZO ZA LAIN ZA SIMU KWA KIASI CHA SHILINGI ELFU MOJA KWA KILA MWEZI LAJA KWA SURA MPYA

‘Vitu vingine ni too cheap (rahisi sana) , hii  kodi ni sheria, jaribuni kufikiria kuwa fedha hii kwa mwezi ni kwa ajili ya kupata maji, barabara  na  mawasi liano’. Makinda  


Wakati sakata la kodi ya simu ya Sh1,000 kwa kila laini ya simu kwa mwezi, inayotakiwa kulipwa na watumiaji wa simu likiwa limerejeshwa bungeni na Serikali, Spika wa Bunge, Anne Makinda ameibuka na kusema fedha hiyo ni ndogo na kila Mtanzania ataweza kuilipa
Spika Makinda alishangazwa na Mtanzania anayeshindwa kupata Sh1,000 kwa mwezi, kufafanua kuwa kama wananchi wataifanya nchi yao kuwa rahisi, watalalamika na umaskini mpaka siku watakayokufa. Julai 30 mwaka huu, Waziri wa Fedha, William Mgimwa alikaririwa akisema suala hilo litamalizwa bungeni kisheria na kwamba wameanza kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete la kuitaka Wizara ya Fedha kukutana na wadau wengine, kuangalia namna ya kupata vyanzo vingine vya mapato mbadala na kodi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa mafunzo ya wajumbe wa kamati ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Bajeti, Spika Makinda alisema, “Haya maendeleo tunayoyataka sisi kama Watanzania yatapatikana kwa kulipa kodi, hata vitabu vitakatifu vinasema kila mtu lazima achangie,”alisema.
Alisema  bila kukusanya kodi nchi itashindwa kujiendesha na kusisitiza kuwa  kama angeulizwa kuhusu masuala ya ulipaji kodi angesema uanzishwe hata mfuko maalumu wa kuwasaidia vijana.
 Alisema kwa kuwa suala hilo la kodi hivi sasa ni sheria, mabadiliko yake ni lazima yarudi bungeni na kwamba haamini katika kushindwa kulipa fedha hiyo. “Tunataka kufanya vitu vingi na hatuwezi kuitegemea Serikali katika kila kitu sasa yenyewe itatoa wapi fedha. Hayo ni maoni yangu lakini hiyo ni sheria,” alisisitiza Spika Makinda

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.