Ads Top

WATANZANIA KUWENI MAKINI KWANI VIBAKA WAGEUKA TISHIO KARIA KOO KUELEKEA MAANDALIZI YA SIKU KUU

  Binti aliyevamiwa na viabaka
 Kibaka akiwa chini ya ulinzi
Maskini binti  kapata kovu bila sababu ya msingi, enyi vibaka, siku zenu zinakaribia.
     Harakati za kujiandaa na sikukuu ya Eid. Kama unavyojua watu kariakoo huongezeka zaidi na vibaka nao hutumia mwanya huo kwaubize wa watu kutafuta mahitaji yao.
 
     Binti mmoja aliyekuwa katika pilikapilika za maandalizi ya sikukuu ya Eid Kariakoo alikutwa na mkasa baada ya kibaka mmoja kutaka kumpora begi lake la mkononi. 
Binti huyo hakuwa tayari kuachia begi lake kirahisi, kitendo ambaacho kilimuudhi kibaka huyo na kumpelekea kumkata na kisu kiganjani binti huyo na kumtishia asipige kelele kwa kuwa atamfanyia kitu mbaya.
   
   Kwa ujasiri aliokuwa kuwa nao binti huyo alipiga kelele zilizopelekea wasamaria wema katika eneo hilo kumsaidia na kumtia nguvuni kibaka huyo eneo la Kariakoo kituo cha mabasi yaendayo Mbagala.
  
   Hatimaye Polisi jamii wakisaidiana na Maaskari wa Usalama barabarani walifika eneo la tukio na kumtia nguvuni kibaka huyo

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.