Ads Top

MBUNGE WA KIGOMA KASKAZINI -CHADEMA ZITTO KABWE:' SOMA TAARIFA YA KUWASILISHA MUSWADA BINAFSI WA SHERIA KUFUTA SHERIA YA MAGAZETI

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe
Nimetoa taarifa rasmi kwa katibu wa Bunge kwa mujibu wa kanuni za Bunge kwamba katika mkutano ujao wa Bunge nitawasilisha muswada binafsi wa sheria kufanya marekebisho ya sheria ya magazeti kwa lengo la kuifuta kabisa sheria hiyo.
Madhumuni ya muswada huo ni;   
“kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 kwa sababu inakinzana na Katiba ya Nchi kuhusu haki za Raia kupata habari na kwamba iliorodheshwa na tume ya Nyalali ni sheria kandamizi’
Muswada wenyewe nitauwalisilisha siku ya ijumaa ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali uweze kuingia kwenye shughuli za Bunge zitakazoanza tarehe 15 Oktoba 2013 kwa ngazi ya kamati.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.