Wanajeshi wa Muungano wa Afrika wakishirikiana na wanajeshi wa Somalia, wameanza mashambulizi mapya dhidi ya kundi la wanamgambo la Al Shabaab
Mwandishi wa BBC nchini humo anasema kuwa wamezindua oparesheni ya
kushambulia ngome mbili zinazotumiwa na wanamgambo hao katika eneo la
Hiraan.
Wanajeshi wa Ethiopia wanaelekea
katika ngome kuu ya wanamgambo hao ya Buloburde, wakati kikosi cha
wanajeshi kutoka Djibouti kikielekea katika ngome ya Bukakable.
Watu wengi wanaripotiwa kutoroka maeneo hayo. Miji mitano ilikombolewa wiki jana kutoka kwa Al shabaab Magharibi mwa Somalia.
Al Shabaab walitumiliwa kutoka mji mkuu
Mogadishi katika mashambulizi makali yaliyofanywa na AU pamoja na
wanjeshi wa Kenya na Somalia.
Hata hivyo wanamgambo hao wamekuwa wakifanya mashambulizi ya kuvizia huku wakilenga hata ikulu ya Rais mjini humo.
Habari na BBCswahili.com
Habari na BBCswahili.com
No comments: