Bao la ushindi la Italy lilifungwa kwa kichwa kupitia mshambuliaji matata Mario Baloteli
Bao la ushindi la Italy lilifungwa kwa kichwa kupitia mshambuliaji
matata Mario Baloteli mda mchache tu baada ya kipindi cha mapumziko.
Awali mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge alikuwa amekomboa bao lililofungwa na Claudio Marchisio wa Italy.
Mechi hiyo ilichezwa chini ya viwango vya juu vya joto katika uwanja wa Manaus uliopo katikati ya msitu wa Amazon.
Katika mechi za awali ,Costa Rica ilitoka nyuma
na kuishinda Uruguay mabao matatu kwa moja huku Colombia nayo
ikiicharaza Ugiriki mabao matatu bila katika mji wa Belo Horizonte.
Wakati huohuo miamba ya soka barani afrika Ivory
Coast imeimarisha matumaini ya bara hili baada ya kutoka nyuma na
kuishinda Japan kwa mabao mawili kwa sufuri.
Ivory Coast ilijipatia mabao yake kupitia
wachezaji Wilfried Bony na aliyekuwa mchezaji wa Arsena Gervinho huku
Japan ikifunga kupitia mshambuliaji wake keisuke Honda.
No comments: