Miamba ya soka barani Afrika Ivory Coast imeimarisha matumaini ya bara hili baada ya kutoka nyuma na kuishinda Japan kwa mabao mawili kwa moja.
Ivory Coast ilijipatia mabao yake kupitia wachezaji Wilfried Bony na
aliyekuwa mchezaji wa Arsenal Gervinho huku Japan ikifunga kupitia
mshambuliaji wake keisuke Honda.
Ushindi huo wa Ivory Coast ni wa
kwanza miongoni mwa timu za bara hili na unaiweka timu hiyo sawa kwa
pointi na Colombia ambayo iliifunga Ugiriki mabao matatu bila jibu.
Ikiwa ni mara ya tatu kwa Ivory Coast kushiriki
katika michuano ya Kombe la dunia,haijawahi kufuzu kupitia michuano ya
kimakundi.
Hatahivyo chombo kilikuwa chaenda mrama baada ya
kocha Sabri Lamouchi kuwashangaza wengi alipomuacha nje aliyekuwa
mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba na kusababisha miamba hiyo kuwa
chini kwa bao moja ilipofikia kipindi cha mapumziko.
Japan ambayo ndio mabingwa wa bara Asia walikuwa
hatari katika ngome ya Ivory Coast kila walipopata mpira na
walifanikiwa kupata bao la kwanza katika dakika ya 16 kutoka
mshambuliaji wao Honda.
Mchezaji huyo wa kiungo cha kati anayeichezea
kilabu ya A.C Milan alipata pasi murwa karibu na lango la upinzani kabla
ya kupiga mkwaju mkali uliomuacha mlinda lango wa Ivory Coast kinywa
wazi.
No comments: