Ads Top

Dk Titus Kamani: Nitakufa na wetendaji watakaochakachua Fedha za mirdi ya maji

 Dk Titus Kamani akikagua mradi wa maji jimbo la Busega

Na Antony Sollo   Busega
WAZIRI wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani, amewaonya watendaji watakaotafuna fedha za miradi mbalimbali inayotekelezwa jimbo la Busega.


 Dk. Kamani, alitoa kauli hiyo jana akikagua mradi wa maji katika kijiji cha Nyangili Kata ya Igalukilo jimbo la Busega Mkoani Simiyu ambapo pamoja na mambo mengine Dk Kamani alikagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Kata hiyo.


Alisema,mradi huo umetumia fedha nyingi ambazo wala si bajeti ya Serikali bali ni juhudi zake binafsi kama mwakilishi wa wananchi hao lakini akiwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo Marafiki ,wahisani pamoja na Benki ya Dunia, “nawaomba ndugu zangu  muulinde mradi huu  na kuhakikisha wananchi wanahudumiwa bila kubaguliwa”

Mradi wa maji katika kijiji cha Nyangili Kata ya Igalukilo jimbo la Busega Mkoani Simiyu umetumia kiasi cha shilingi milioni 300,000,000.ikiwa ni fedha kutoka Benki ya Dunia.


Najua mmepata shida hii ya maji kwa muda mrefu hatimaye serikali yenu imesikia kilio chenu, hivyo kuuharibu au kuuchakachua mradi huu ni kutaka muendelee na shida iliyokuwa inawasumbua na ninaapa,nitakufa na watu watakaofuja fedha za miradi inayotekelezwa katika jimbo letu.


Dk Kamani ameitaja miradi inayotekelezwa katika kata ya Igalukilo kuwa  ni pamoja na mradi wa Umeme unapita katika kijiji cha Nyangili,Lunala na Mwamagigisi,na mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa Kituo cha Afya Igalukilo.


Upande wa ujenzi wa barabara,Dk Kamani alisema kuwa miradi ya barabara imetengewa shilingi milioni 300,000,000. Ambapo alisema barabara ya Mwamjulila na badugu itatengenezwa na itapitika kwa urahisi kuliko ilivyokuwa hapo awali kabla ya Uongozi wa Dk Kamani.


Baada ya kukagua miradi mbalimbali katika kata hiyo Dk Kamani alihutubia Mkutano wa hadhara katika kijiji cha Malangale ambapo aliwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumpigia kura na kumpa ushindi na kuwaahidi kuwa ataendelea kutimiza ahadi pamoja na kutekeleza ilani ya chama kwa kuwaletea maendeleo ya pamoja,badala ya kushughulika na mtu mmoja mmoja.


Dk Kamani aliguswa na Risala ya kikundi cha wananchi kinachojulikana kama fogong’ho ambacho kinafanya shughuli za kuchangiana na kukopeshana fedha kwa ajili ya kujinunulia mahitaji madogomadogo ambapo alitoa mchango wa shilingi laki tano500,000. kuunga mkono juhudi za wanakikundi hao.


Akihitimisha hotuba yake,Dk Kamani alitoa mpira kwa wachezaji wa timu ya Zege Malangale FC na kuwaasa kuwa,michezo ni Afya hivyo ili waweze kuwa na Afya njema wajitahidi kushiriki Michezo mbalimbali ikiwemo mpira wamiguu,riadha,mbio za baiskeli na michezo mingine ili kuzilinda Afya zo.


Akizungumzia watu wanaopita kufanya kampeni chafu jimboni Dk Kamani alisema,ndugu zangu wananchi wa Malangale, kuweni macho na watu wanaopita kuwarubuni,maendeleo hayatapatikana kwa kugawiwa fedha kwa mtu mmoja mmoja bali nawashauri kuwa fursa ziko nyingi hebu undeni vikundi vya ushirika ili Serikali iweze kuwapa ruzuku katika shughuli za Uvuvi.


“Serikali kwa sasa inatoa ruzuku ya asilimia arobaini ( 40 ) kwa wanaushirika wa vikundi vya Uvuvi ili ziwasaidie kununua mitumbwi na Nyavu kwa ajili ya shughuli za Uvuvi changamkieni fursa hii kwani mimi niko tayari kuwaonyesha njia ili muweze kunufaika na sekta hii ambayo iko katika eneo lenu.alisema Dk Kamani.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.