KUTOKA: JESHI la Polisi Kanda ya Dar es Salaam linawashikilia na kuwahoji watu wanane kwa kutupa viungo vya binadamu katika bonde la Mbweni Mpiji eneo la Bunju wilayani Kinondoni
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaan Suleiman Kova
JESHI la Polisi Kanda ya Dar es Salaam
linawashikilia na kuwahoji watu wanane kwa kutupa viungo vya
binadamu katika bonde la Mbweni Mpiji eneo la Bunju wilayani Kinondoni .
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam Suleiman Kova amesema hayo leo Ofisi kwake wakati wa mkutano na
waandishi wa habari .
Amesema kuwa watu hao wakimemo madaktari wa
International Medical and Technological University (IMTU) wanashikiliwa
na Jeshi la Polisi baada ya kukiri kuhusika na tukio la utupaji wa
viungo vya binadamu katika eneo hilo.
Kamishna Kova amesema kuwa Jeshi la Polisi
linaendelea kuwahoji na kufanya uchunguzi kuona kama wahusika wamefanya kosa
linalohitaji kuchukuliwa hatua za kisheria au hawana kosa.
Ameongeza kuwa kufuatia tukio hilo tayari Jeshi
la Polisi Kanda Maalum limeshafungua jarada la uchunguzi kubaini ikiwa wahusika
wametenda kosa linalohitaji kufikishwa kwenye vyombo vya sharia kwa hatua
zaidi.
Kamishna huyo amesema kuwa katika kutekeleza
jambo hilo tayari jopo la wachunguzi likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Kanda
Maalum ya Dar es Salaam Jaffar Mohamed linaendelea na uchunguzi ili
kubaini chanzo cha watu hao kutupa viungo hivyo katika eneo hilo na idadi ya
watu kulingana na viungo vilivyotupwa.
Aidha Kamishna Kova amewasihi wananchi wasiwe na
wasiwasi kwani viungo vilivyookotwa havina uhusiano na mauaji ya watu
wengi na wala havihusiki na masuala ya ushirikina.
Amewaahidi wananchi kutoa taarifa kamili mara tu
upepelezi utakapokamilika.
Viungo vya binadamu vikiwemo mikono, miguu,
vichwa , mapafu na mioyo viligundulika jana (21.7.2014) jioni vikiwa
vimehifadhiwa katika mifuko ya plastiki 85 na kutupa katika bonde la Mbweni
Mpiji eneo la Bunju wilayani Kinondoni.
Mara baada ya kugunduliwa Jeshi la Polisi Mkoa
wa Kipolisi wa Kinondoni walivichukua na kuvipeleka katika Hospitali ya Taifa
kwa uchunguzi zaidi.
No comments: