Ads Top

Afrika Kusini imefufua matumaini yake ya kufuzu kwa raundi ijayo ya michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini



Wachezaji wa Afrika Kusini

kwa magoli mawili kwa bila, katika mechi yaon ya pili siku ya Jumatano.
Vijana hao wa Bafana Bafana walianza mechi hiyo vyema kuliko walivyocheza katika mechi yake ya ufunguzi dhidi ya Cape Verde.
Katika kipindi cha kwanza ilifanya mashambulizi kadhaa katika lango la Angola.
Kunako dakika ya kumi na tano Afrika nusura ifunge bao lakini msaidizi wa refa wa mechi hiyo aliinua kijibendera kuashiria kuwa alikuwa ameotea.
Dakika mbili baadaye Bafana Bafana ilifanya shambulio lingine na mkwaju wa Siyabonga Sangwen ulikosa gola kwa ncha.

Wachezaji wa Afrika Kusini wakisherehekea bao lao
Kunako dakika ya 30 Siyabonga Sangweni akaifungia Afrika Kusini bao lake la kwanza.
Bao hilo lilionekana uwapa nguvu wachezaji wa Afrika Kusini ambao waliendeleza mashambulio yao dhidi ya Angola.

Malalamiko ya kocha

Afrika Kusini ingelifunga magoli zaidi katika kipindi hicho lakini wachezaji wake kadhaa walikosa umakini wakati wa kumalizia kwa kupoteza pasi nzuri walizopewa na wakati mwingine kupiga mpira ovyo.
Hata hivyo juhudi zao hazikufanikiwa na kufikia wakati wa mapunziko Afrika Kusini ilikuwa ikiongoza kwa bao moja kwa bila.
Kabla ya mechi hiyo kocha wa Afrika Kusini alikuwa amewashutumu wachezaji wake kwa kukosi umakini wakati wa mechi muhimu na inaonekana kuwa mazungumzo yake na wachezaji wake imeonekana kuzaa matunda.
Kipindi cha pili kilianza huku Angola ikiwa na wachezaji kumi pekee baada ya refa wa mechi hiyo kuanza mpira kabla ya kuruhusu mabadiliko katika kikosi cha Angola.
Kinyume na iliyokuwa katika kipindi cha kwanza wachezaji wa Angola walianza kuonana na kufanya mashambulio kadhaa katika lango la Afrika Kusini.
Lakini, licha ya juhudi hizo, Afrika Kusini ilipata bao lake la pili kunako dakika ya 61 kupitia kwa mchezaji wake wa ziada Lehlohonolo Majoro, ambaye alikuwa ameingia uwanjani dakika mbili tu kabla ya kufunga bao hilo.
Mshambulizi matata wa Angola, Manucho ambaye alitarjiwa kukiongoza kikosi chake kushinda mechi hiyo, alithibitiwa na zaidi ya wachezaji wawili wa Afrika Kusini, mara tu alipopewa pasi.
Angola sasa ni sharti ishinde mechi yake ya mwisho dhidi ya Cape Verde siku ya Jumapili na iombe Morocco itoke sare na Cape Verde katika mechi yao ya Jumatano ili iweze kufuzu kwa hatua ya robo fainali.
Hata hivyo huenda maombi hayo yasitimie ikiwa kutakuwa na mshindi wa mechi ya leo na hivyo Angola italazimika kusubiri matokeo ya mechi kati ya Afrika Kusini na Morocco siku ya Jumapili ili kufahamu ikiwa imeyaaga mashindano hayo au la

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.