Morocco yatoka sare na Cape Verde
Cape Verde imeandikisha historia
kwa kufunga bao lake la kwanza katika fainali za mataifa ya Afrika
yanayoendelea nchini Afrika Kusini.
Cape Verde, amabyo inashiriki katika fainali
hizo kwa mara ya kwanza imetoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na
mabingwa zamani wa kombe hilo Morocco, katika mechi ya nne ya kundi
A.
Cape
Verde, ilipata bao lake kunako dakika ya 36 kupitia kwa nyota wake
Platini, ambaye alipokea pasi nzuri kutoka kwa mshambulizi Ryan Mendes
Morocco, ilianza mechi hiyo ikiwa na matumaini
makubwa ya kuimarisha nafasi yake ya kusonga mbele kwenye mashindano
hayo, kwa kunadikisha ushindi wao kwa kwanza.
Nyota wa Morocco, Younes Belhanda, wa klabu ya Montepilier ni miongoni mwa wachezea wa Tunisia katika mechi hiyo.
Belhanda alijumuishwa katika kikosi hicho ili
kuimarisha safu ya mashambulizi baadaya wa Morocco kutoka sare mechi
yake ya ufunguzi.
Cape Verde yapania kushinda mechi yake ya kwanza
Ila tangu kipenga cha mwanzo, Cape Verde ilionekana kuilemea miamba hao wa Afrika Kaskazini.
Kocha wa Cape verde Luis Antunes, ana matumaini
makubwa kuwa kikosi chake ambacho kinashiriki katika mashindano hayo kwa
mara ya kwanza watashinda mechi hiyo.
Juhudi za Morocco kusawazisha katika kipindi cha kwanza hazikufua dafu.
Dakika za kwanza arubaini na tano zimekamilika na Cape Verde iko kifua mbele kwa bao moja kwa bila.
Lakini kunako dakika ya sabini na nane Morocco ilizawazisha na kufanya mambo kuwa moja kwa moja.
Cape Verde, sawa na Morocco, ilitoka sare ya
kutofungana bao lolote katika mechi yao ya ufunguzi, lakini ilionyesha
mchezo mzuri kuliko wapinzani wao Afrika Kusini.
Afrika Kusini inaongoza kundi hilo la alama nne
na inahitaji kutoka sare mechi yake ya mwisho ya makundi ili kufuzu kwa
robo fainali ya mashindano hayo.
Cape Verde na Morocco zinashikilia nafasi ya pili na alama mbili kila mmoja huku Angolo ikivuta mkia.
Timu hizo tatu sasa ni sharti zishinde mechi zao za mwisho ili kufuzu kwa robo fainali ya mashindano hayo.
Siku ya Alhamisi Mali inacheza na Ghana kisha Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoa udhia Niger
]katika mechi za kundi B
Kikosi cha Morocco | Kikosi cha Cape Verde |
01 Lamyaghri 02 Chakir 03 Bergdich 05 Benatia 17 El Adoua 07 Barrada 08 El Ahmadi 10 Belhanda 11 Assaidi 14 El Hamdaoui 21 Amrabat Wachezaji wa ziada 01 Lamyaghri 02 Chakir 03 Bergdich 05 Benatia 17 El Adoua 07 Barrada 08 El Ahmadi 10 Belhanda 11 Assaidi 14 El Hamdaoui 21 Amrabat |
01 Vozinha 03 Varela 06 Neves 08 Varela 14 Gege 18 Nivaldo 05 Babanco 07 Platini 15 Soares 11 Tavares 20 Ryan Wachezaji wa Ziada 12 Fock 16 Rilly 13 Lima 19 Pecks 23 Carlitos 02 Stenio 04 Ramos 17 Souto 22 Silva 09 Rambe 10 Heldon 21 Djaniny |
No comments: