CHAMELEONE HUENDA AKAFUNGULIWA KESI YA MAUAJI
Joseph Mayanja aka Chameleone na mkewe Daniella Atim.
POLISI nchini Uganda wanaendesha uchunguzi ambao huenda wakamfungulia
mashitaka ya mauaji mwanamuziki ‘chakaramu’, Joseph Mayanja aka
Chameleone, mkewe Daniella Atim na kundi la muziki la Leon Island.
Marehemu Robert Karamagi akiwa katika Hospitali ya Mulago baada ya kukumbwa na majeraha nyumbani kwa Chameleone.
Hii ni kutokana na kifo cha Robert Karamagi, 27, aliyefariki katika
Hospitali ya Mulago baada ya kukumbwa na majeraha aliyoyapata nyumbani
kwa mwanamuziki huyo huko Seguku.
Akihojiwa na gazeti la Sunday
Vision, Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kajjansi, Ibrahim Saiga, alisema
wamechukua ushahidi mbalimbali kutoka kwa majirani na mashuhuda
walioona, ushahidi ambao unapingana na ule uliotolewa na familia ya
Mayanja.
Pamoja na kusema kwamba faili la uchunguzi huo litapelekwa
kwa Mwendesha Mashitaka wa Serikali (DPP) kwa ushauri, Saiga alisema
baba wa Karamagi alikana kwamba mwanaye alijimwagia mafuta na kujiwasha
moto.
Pia alisema kwamba mwanaye huyo alimwita kwenda hospitalini
hapo ambapo alimwambia alikuwa ameteswa, akafungwa kamba, akamwagiwa
mafuta na kuchomwa moto na mwanamuziki huyo na wenzake wa kundi lake.
Alhamisi iliyopita, Chameleone alihojiwa na wapelelezi kwa muda mrefu, lakini aliachiwa kwa dhamana.
No comments: