Ads Top

WANANCHI MLANDIZI WALALAMIKIA UTENDAJI WA JESHI LAPOLISI

  Bwana Ally akionyesha kidole chake kilichokatwa na mapanga walipovamiwa katika tukio hilo
majeraha mkono wake wa kushoto ambapo umepinda baada ya kushambuliwa na majambazi
Mguu wa mjukuu wa mwenyekiti huyo Nusura Karim uliokatwa panga katika tukio hilo
Mme wa M.kiti huyo Bwana Ally Ngwallu akiwa na majeraha kichwani baada ya kukatwa katwa kwa mapanga katika tukio hilo
Mtoto huyo akiwa na Babu yake
Mwenyekiti akiwa na makovu baada ya kukatwa mapanga mapanga 
 
 Watishia kuwashtaki watendaji wa Jeshi hilo kwa IGP 
Kesi zikifunguliwa watuhumiwa huachiwa katika mazingira tata Ni pamoja na za Unyang’anyi wa kutumia silaha

Na Antony Sollo Kibaha
Jeshi la Polisi kituo cha Mlandizi Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani limeendelea na kigugugmizi katika masuala mbalimbali ikiwemo kushindwa kusimamia majukumu ya kuanzishwa kwa jeshi hilo  yaani kulinda raia na mali zao
Akiongea kwa huzuni kubwa mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Abdalla mkazi wa kitongoji cha Msongola kata ya Janga amesema tumesikitishwa sana na utendaji wa jeshi la polisi kwa kushindwa kusimamia majukumu yake hususani kulinda raia na mali zao,hii inatokana na matukio mbalimbali yaliyotokea miezi michache iliyopita lakini pamoja na Jeshi hilo kupatiwa taarifa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa hadi leo.
Matukio hayo ni pamoja na kuvamiwa kukatwakatwa kwa mapanga Mwenyekiti wa Kitongoji chetu  Nusura Ngwallu pamoja na familia yake tukio ambalo liliripotiwa kituoni hapo lakini hadi sasa hakuna hatua zilizochukuliwa na jeshi hilo tukio ambalo limepelekea kujeruhiwa vibaya kwa wanafamilia hao na watu watuhumiwa walipokamatwa mara ya kwanza walihojiwa na kukiri kuwa walitumwa na mtu ambaye anadaiwa kuwa ana mgogoro wa maeneo na wananchi wa kitongoji hicho huku mwenyekiti wa kitongoji hicho akisimamia Haki za raia ambazo zilitaka kuporwa na mwekezaji huyo lakini maajabu hadi leo hawajafunguliwa kesi yoyote na jeshi hilo.
Zipo tuhuma mbalimbali zinazomlenga moja kwa moja Mkuu wa kituo cha Polisi Mlandizi kwa kutuhumiwa kutumiwa na wafanyabiashara mbalimbali na wawekezaji  kwa lengo la
  kuwakumbatia katika matukio mbalimbali  hii ni pamoja na kujiingiza katika migogoro  ya Ardhi katika maeneo hayo ambapo kuna kesi mbalimbali ambazo hazifunguliwa mpaka sasa huku taarifa zikidai kuwa watuhumiwa wa kesi hizo wamekamatwa na kuachiwa hivyo kutofikishwa mahakamani.
Mwandishi wa Habari alimtafuta Mwenyekiti wa Kitongoji cha Msongola ili kujua ukweli wa tuhuma zinazolikabili Jeshi la Polisi Wilayani Kibaha ambapo alikuwa na haya.
Ndugu mwandishi mimi kwa jina naitwa Nusura Ngwallu ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Msongola Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani tukio  la kuvamiwa na kukatwa katwa na mapanga lilitokea jumatatu tarehe 02/10/2012 majira ya saa 7 usiku hapa nyumbani kwangu na ripoti katika kituo cha polisi Mlandizi na watu waliofanya tukio hilo baadhi yao tuliwatambua na hadi sasa waliachiwa tu na wanaendelea kutamba mtaani jambo linalotuondolea imani na jeshi la polisi maana kigugumizi cha kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha mahakamani kinaonyesha wazi udhaifu mkubwa katika utendaji wa Jeshi hili.
Ndugu mwandishi inashangaza kuitwa mahakamani na kukuta washtakiwa hawajafunguliwa kesi yoyote najiuliza hivi kweli watendaji wa jeshi la polisi katika kituo cha polisi Mlandizi wanajua vizuri wajibu wao au wamejaa ubabaishaji na maslahi binafsi!
Inasikitisha sana juzi nimeletewa ujumbe kuna mtu anadai kuwa iwapo nitaendelea kusimamia msimamo wangu katika mgogogro wa Ardhi kati ya wananchi na Mwekezaji safari hii nitauawa maana kuvamiwa kwangu kumbe sijajifunza kitu.
Nimeshangazwa na kuanza kuandamwa mpaka na viongozi wa Chama changu kwamba siwajibiki huku wakijua kuwa ninaumwa na taarifa ya Daktari ipo na ameshauri nipumzike mpaka nitakapopona ili niendelee na majukumu yangu ambapo sasa inaonekana baadhi yao
wanatumiwa ili kuniondoa katika nafasi hii ili wafanikishe uporaji wa Ardhi ya wananchi. 
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Msongola Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Nusura Ngwallu umri wa miaka 43 hadi sasa anatishiwa kuuawa na watu wanaodaiwa kuwa wametumwa na mwekezaji aliyepora maeneo ya wananchi wa kitongoji cha Msongola Wilaya ya
Kibaha Mkoani Pwani ambapo tukio hili la kuvamiwa na kukatwa na mapanga yeye na mme wake pamoja na mjukuu wao Nusura Karim umri wa miaka  2 lilitokea jumatatu tarehe 02/10/2012 majira ya saa 7 usiku huko nyumbani kwake na ripotiwa katika kituo cha polisi Mlandizi lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kwa watu wanaotuhumiwa kumvamia mwenyekiti huyo kwa lengo la kumuua yeye na mme wake Bwana Ally Ngwallu mwenye umri wa miaka 53 wote wakazi wa Kitongoji cha Msongola.
Mkuu wa Kituo hicho alipotafutwa kujibu tuhuma zinazotolewa na wananchi hao akiwemo mwenyekiti wa Kitongoji hicho simu yake ilikuwa ikitumika muda wote ambapo juhudi za kumtafuta zinaendelea

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.