HOFU YA JANGA LA KIBINADAMU MASHARIKI YA KATI
Kambi ya wakimbizi nchini Syria
Shirika la kutoa misaada la International Rescue Committee, limeonya
kuwa eneo la Mashariki ya kati linakabiliwa na Janga kuu la kibinadamu
kutokana na Vita vya Syria.
Shirika hilo sasa linatoa mwito wa msaada mkubwa zaidi kutolewa na
jamii ya kimataifa likisema ule
uliotolewa kufikia sasa hautoshelezi
kamwe.
Takriban watu millioni mbili wameachwa bila makao nchini Syria.
Shirika hilo linaongezea kuwa masaibu ya ubakaji
ni miongoni mwa mambo yanayoandamana na Vita hivyo vya wenyewe kwa
wenyewe na ambalo hutekelezwa mbele ya Familia za Waathiriwa.

Tanzanian Shilling Converter
No comments: