Mechi ya mwisho ya makundi kati ya Togo na Tunisia
Mechi ya mwisho ya makundi kati ya Togo na
Tunisia, inakisiwa kuwa moja ya mechi ngumu zaidi katika fainali za
mashindano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika mwaka huu.
Hii
ni kutokana na kuwa timu hizo mbili zina alama mbili kila mmoja naTogo
inahitaji ushindi ili kufuzu kwa hatua ya robo fainali nayo Tunisia
ikihitaji sare ya aina yote ili isonge kwa hatua ijayo.
Togo ilianza mechi hiyo kwa vishindo huku
ikipata bao lake la kwanza kunako dakika ya 12 kupitia kwa mchezaji
Serge Gakpe ambaye alipokea pasi nzuri kutoka kwa nahodha wa timu hiyo
Emmanuel Adebayor.
Emmanuel Adebayor ndiye anayetarajiwa kuongoza
kikosi cha Togo katika harakati zao za kufuzu kwa robo fainali ya
mashindano hayo kwa mara ya kwanza.
Tangu miaka minane iliyopita, Adebayor amekuwa
mmoja wachezaji muhimu zaidi katika kikosi cha Togo, lakini uhusiano
wake wa maafisa wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Togo, haujakuwa
wa kuridhisha.
Togo haijawahi kufuzu kwa robo fainali ya
mashindano hayo, na ikiwa itafanikiwa katika mechi ya leo basi itakuwa
imeandikisha historia
No comments: