Miezi 18 katika chumba cha kuhifadhia maiti
Fortune Adzawoloo, alifariki mwaka 2011
Mwili wa raia wa Ghana
aliyekuwa anafanya kazi ya uvuvi Ireland Kaskazini , bado uko kwenye
chumba cha kuhifadhia maiti, zaidi ya mwaka mmoja baada ya kifo chake.
Juhudi za kutaka kuurejesha mwili wake nyumbani kwao mazishi hadi kufikia sasa hazijafanikiwa.
Fortune Adzawoloo, 29, alifariki mwezi Julai mwaka 2011, wiki sita baada ya kuanza kazi yake ya uvuvi.
Familia yake, inataka mwili wake kurejeshwa nyumbani lakini wanazozana kuhusu nani atagharamia safari hiyo.
Bwana Adzawoloo alipelekwa hospitalini tarehe 18 mwezi Julai mwaka 2011, lakini akafariki baadaye siku hiyo.
No comments: