Al Shabaab wadai kumuua Mkenya
Wanamgambo wa Al
Shabaab wanadai kumuua mateka Mkenya awaliyekuwa wanamzuilia baada ya
Kenya kukosa kutimiza matakwa yao.
Al Shabaab wanaitaka serikali ya Kenya kuwaachilia huru waisilamu wanaozuiliwa nchini humo kwa tuhuma za ugaidi.
Wanamgambo hao, wanaotaka kutekeleza
sheria za kiisilamu pia walisema kuwa wanaongeza makataa ya kuwaua
mateka wengine wakenya kwa masaa 72 kuipa muda Kenya kutimiza matakwa
yao.
Mapema mwezi Januari, wanamgamba hao walipatia
Kenya makataa ya wiki tatu kuwaachilia wafungwa hao , lakini Kenya
ikakataa kutimiza.
Kabla ya makataa hiyo kutolewa, wanamgambo hao
walimuua mwanajeshi wa Ufaransa, waliyekuwa wanamzulia kama hatua ya
kulipiza kisasi kile wanachosema ni mateso yanayofanyiwa na Ufaransa
dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu Mali.
kwa habari zaidi bofya hapa...>>>>>
kwa habari zaidi bofya hapa...>>>>>
No comments: