Ads Top

TAIFA STARS YAIBUKA NA USHINDI ZIDI YA TIMU YA TAIFA YA MOROCCO KATIKA MECHI YAKE YA KUFUZU KUCHEZA KOMBE LA DUNIA MWAKANI NCHINI BRAZIL

 Wachezaji wa Taifa Stars wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na Thomas Ulimwengu.

TIMU ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo imeishushia kichapo timu ya taifa ya Morocco baada ya kuilaza kwa mabao 3-1 kwenye mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Taifa Stars yamefungwa na wachezaji wa TP Mazembe, Mbwana Samatta aliyetupia kambani bao mbili na Thomas Ulimwengu aliyefunga bao moja. Mchezo huo ulikuwa wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.