Ads Top

Waziri wa afya wa Afrika Kusini: Amesema kuwa zaidi ya asili mia 28% ya wasichana wa shule wameambukizwa virusi vya Ukimwi


wasichana wengi waathirwa na HIV nchini Afrika Kusini 
Waziri wa afya wa Afrika Kusini Amesema kuwa zaidi ya asili mia 28% ya wasichana wa shule wameambukizwa virusi vya Ukimwi, ikilinganishwa na asili mia 4% tu ya vijana wa shule.
Hii ameelezea ni kutokana pakubwa na kuongezeka kwa mababa sukari au kwa jina lingine, *fataki*, ( Wazee wanao tembea na wasichana wadogo kwa umri).
Waziri Aaron Motsoaledi amesema kuwa wamepata ushahidi kuwa wasichana wengi wamejiingiza katika mapenzi na wazee waliowazidi ki umri badala ya kuwa na vijana wa rika lao.
Takwimu za punde zaidi zimeonyesha kuwa asili mia kumi ya raia wa Afrika Kusini wanaishi na virusi vya HIV. Nchi hiyo imekuwa na mradi wa kuvuma zaidi wa kutoa dawa za kukabili makali ya virusi hivyo vya HIV , ARV tangu rais Jacob Zuma alipomteua bwana Motsoaledi kuongoza wizara hiyo ya afya yapata miaka minee iliyopita. Kwa habari zaidi bofya hapa..>>>>

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.