Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema Mh John Mnyika Amshtaki Naibu Spika Job Ndugai Kwa Wapiga Kura Wake
Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema Mh John Mnyika
Na Bryceson Mathias, Iyegu Kongwa
MBUNGE
wa Jimbo la Ubungo na Kiongozi wa Kitaifa wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), John Mnyika, amemshitaki Naibu Spika wa Bunge la
Tanzania Job Ndugai kwa wapiga kura wake, akiwahoji iwapo walimtuma
bungeni kufanya Ubabe wa kuwatoa nje wabunge wenzie badala ya kuwatetea.
Mnyika
alitoa Mashitaka hayo leo Aprilli 26, 2013 katika kijiji cha Iyegu,
Kata ya Mlali, Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, ambapo alisema amemkatia
Rufaa Ndugai mara Tano bungeni bila majibu, kwa hiyo jana aliamua
kumshitaki kwao ili wafanye maamuzi magumu juu ya mbunge wao asiyefanya
kazi waliyomtuma.
Akizungumza
katika Mkutano huo Mnyika alimshitaki Ndugai akiwahoji kama walimtuma
kufanya hivyo, na waliposema Laa, aliwataka kufanya mabadiliko ya
mwakilishi wa Jimbo lao kama wanataka kumaliziwa Kero zao zikiwepo ni
Haki na Maendeleo ya kiuchumi na Matumizi bora ya Rasilimali zao.
Mwananchi
mmoja alimhoji Mnyika “Je, ni nani aliyetayarisha, kulinda, kusimamia
na kusafirisha Twiga wetu kwenda nje, lini watarejeshwa na waliohusika
watafanywaje?.
Mnyika
aliwajibu wananchi kwamba, wahusika wa usafirishaji wa Twiga wao
ni vigogo walioko madarakani, na Twiga hao wako nchi mmoja ya Kiarabu,
na mbali ya Twiga hao hivi karibuni Chadema itaibua suala la Tembo, na
kuwaambia suluhisho la haraka yote hayo ni kufanya mabadiliko ya
viongozi mafisadi.
Alipoulizwa
Mauaji na Vitisho wanavyofanyiwa na Kundi linalojiita Kanyaga
Twende, wanapoamua kujiunga na Upinzani, Mnyika aliwauliza kama wanayo
simu ya Mbunge wao wamuulize wasimtukane, na waliposema hawana
aliwatajia namba ya Ndugai na ya Mkurugenzi wa Usalama Chadema
atakayewasaidia kwa vitisho .
Aidha
Mnyika kabla ya kushuka Jukwani saa 11.30 jioni, aliuuliza umati
uliokuwepo wangapi wapo tayari kwa mabadiliko ya M4C, watu wote karibu
1,000 walinyosha mikono na Mnyika akashuka kuelekea Kongwa kuungana na
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje, kuendelea na Mkutano.
No comments: