Ads Top

TANGA:Wafanyabiashara na wakazi wa jijini Tanga, wameiomba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupunguza bei za ving’amuzi

 
Kutokana na watu wengi kushindwa kumudu gharama zake.
TCRA, ilizima mitambo yake ya anolojia na kuwasha ya digitali Februari Mosi mwaka huu kwa Mkoa wa Tanga na kuwafanya watu wengi kukosa fursa ya kupokea matangazo na kupata habari.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wengi waliilalamikia TCRA kwa kuruhusu ving’amuzi kuuzwa kwa bei kubwa.
Waliishauri Mamlaka ya Mawasiliano kupunguza bei ya ving’amuzi ili nao waweze kupokea matangazo katika televisheni zao kwani kwa sasa zimebaki mapambo ndani ya majumba yao.
Bakari Mfaume ambaye ni mkazi wa Mwahako, alisema Mamlaka ya Mawasiliano inapaswa kusimamia bei za ving’amuzi pamoja ili bei yake iweze kuwa nafuu kwa watu wengi.
Akizungumzia kuhusu mazoea ya kupokea matangazo na kupata habari kupitia televisheni zao, mkazi wa Sahare, Makame Kombo, alisema sasa Watanzania wanarejeshwa kutoka zama za ukoloni ambako walishasahau na hivyo kuitaka Serikali kuingilia kati.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.