Ads Top

Mamia ya Watu Walivyojitokeza Wakati Mwili wa Msanii Albert Mangwea Ulipowasili Jana Mkoani Morogoro Jana Kwa Ajili ya Mazishi Leo

  Sehemu ya pikipiki na umati wa watu waliokuwa pembezoni mwa barabara kushuhudia msafara huo.
  Abiria waliokuwa wakisafiri na Basi la Aboud, wakiwa wameteremka chini baada ya magari yote yaliyokuwa yakielekea jiji Dar kutoka Morogoro kuzuiliwa kwa muda ili kupisha msafara wa magari yaliyokuwa yakiongozana na msiba wa Msanii Albert Mangwea, wakati ukiwasili mjini Morogoro  jana jioni, ambapo umati wa watu ulijitokeza kuanzia Mikese kwa ajili ya kumpokea huku msafara huo ukidakwa na mapikipiki yapatayo kama 500 yaliyoanza kuongoza msafara huo kuelekea nyumbani kwa wazazi wa marehemu huku ulinzi ukiimarishwa zaidi kila kona ya mji huo wakati msafara huo ulipowasili.
  Askari wa usalama barabarani, akiongoza magari hayo wakati yakiwasili mjini Morogoro jana jioni kwa ajili ya mazishi leo
 Msafara huo ukipokelewa na Pikipiki maarufu kama Bodaboda zilizoanza kuongoza msafara huo kwa mwendo wa pole hadi nyumbani kwa marehemu
 Msanii Afande Sele, akiwapokea wageni waliowasili na msafara huo.....
  Askari akitanga kiatu alichokiokota baada ya raia kusukumana eneo hilo wakigombea kuona jeneza lenye mwili wa marehemu.
Ulinzi pande hizi za nyumbani uliimarishwa kama hivi.Picha zote na Sufiani Muhidini

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.