Mjukuu wake Nelson Mandela, Mandla , amewatuhumu jamaa zake kuwa na njama ya kutaka udhibiti wa mali ya babu yake rais wa zamani wa Afrika Kusini
Mandla Mandela
Matamshi yake yanakuja baada ya mahakama kuamuru kuwa mabaki ya
wanawe Mandela kufukuliwa na kuzikwa nyumbani kwa Mandela katika kijiji
cha Qunu.
Mnamo Jumatano polisi walifukua
mabaki ya wanawe Mandela nyumbani kwa Mandla kufuatia agizo la mahakama
baada ya kuwasilisha malalamiko yao mahakamani.
Mandela, mwenye umri wa miaka 94, yungali hali mahututi hospitalini lakini madaktari wamedhibiti hali yake.
Rais Jacob Zuma alitoa taarifa baada ya kumtembelea mzee Mandela hospitalini mjini Pretoria.
Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya
familia ya Mandela juu ya urithi wake lakini imekithiri huku hali yake
ya kiafya ikiendelea kuwa mbaya zaidi.
Mzozo huu wa hivi karibuni kuhusu makaburi unatokana na hoja ya wapi azikwe Mandela akifariki.
Stakabadhi zilizowasilishwa mahakamani wiki jana zilionyesha kuwa anatumia mashine ya kupumua.
Alilazwa hospitalini tarehe 8 mwezi Juni baada ya kuugua maradhi ya mapafu.
Mkewe amesema kuwa Mandela wakati mwingine anasumbuka lakini hajalalamika kusema anahisi uchungu wowote.

Tanzanian Shilling Converter
No comments: