Ads Top

Watendaji Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Wapewa Mafunzo ya Bajeti Kijinsia

 Meza kuu ikiwasilisha hotuba zake kwa washiriki wa mafunzo.
Mkurugenzi wa Mashirika yasio ya Kiserikali toka wizara hiyo, Marcel Katemba akisoma hotuba ya Katibu Mkuu
Mkurugenzi wa Mashirika yasio ya Kiserikali toka wizara hiyo, Marcel Katemba akizungumza kabla ya kufungua mafunzo.
 Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo hayo ya kijinsia
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada anuai.
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada anuai.
 Baadhi ya washiriki wa semina hiyo

Watendaji Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Wapewa Mafunzo ya Bajeti Kijinsia .

Na Mwandishi wa Thehabari.com
VIONGOZI wakuu na watendaji wa idara mbalimbali kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto nchini leo wamepewa mafunzo ya namna ya kuandaa bajeti kwa kuzingatia usawa wa kijinsia.

Mafunzo hayo ya siku nne yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yameandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kupitia taasisi yao ya Chuo cha Jinsia (GTI), ambapo washiriki hao kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wanawezeshwa kuandaa bajeti kwa mtanzamo wa kijinsia.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa kuwa yanasaidia kujenga stadi na maarifa kwa viongozi na watendaji wakuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kuzingatia masuala ya jinsia kwenye bajeti ya Wizara hiyo.

Alisema ni mafunzo yanayounganisha utashi wa kisiasa kwa kuzingatia masuala ya jinsia na usawa serikalini, ili kupunguza mapengo yaliyopo inabidi kuwekeza fedha na rasilimali anuai.

alisema nadharia iliyopo kwenye sera inaweza kutekelezeka endapo kutakuwa na uwezeshaji wa rasilimali na fedha ili kuhakikisha huduma za kijamii zinatekelezwa kwa kuzingatia mahitaji ya makundi yote yaani wanawake na wanaume. 

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.