Wabunge nchini Kenya wanatarajiwa kukutana kwa dharura hii leo kujadili ikiwa nchi hiyo itajiondoa kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC au la
Hatua hii ya wabunge inakuja zaidi ya wiki moja kabla ya kuanza kwa
kesi dhidi ya naibu Rais wa Kenya Williiam Ruto kuhusiana na ghasia za
baada ya uchaguzi mwaka 2008.
Ruto anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Rais Uhuru Kenyatta pia anatarajiwa kufika katika mahakama hiyo mwezi Novemba kuhudhuria kesi dhidi yake.
Wawili hao wanashtakiwa kwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi mwishoni mwa mwaka 2007.
Msemaji wa ICC ameambia BBC kuwa kesi hiyo
itaendelea hata ikiwa Kenya itajiondoa kwenye mkataba wa Roma
uliopelekea kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Bwana Fadi El Abdallah, alisema kuwa itachukua
karibu mwaka mmoja kwa mchakato wa nchi yoyote yoyote ile kujiondoa
kutoka katika mahakama ya ICC na hii bila shaka inaathiri tu kesi
zilizokuwa mbele ya mahakama hiyo kwa wakati huo. habari kutoka BBC Swahili
No comments: