Ads Top

Serikali yaendelea kuhimiza matumizi ya mashine za EFDs nchini.

Waziri Mkuu Pinda akisisitiza jambo
Serikali yaendelea kuhimiza matumizi ya mashine za EFDs nchini.

Nashawishika, natambua na nimejiridhisha kuwa elimu kwa mwanadamu ni mwanga na nuru ya maisha, mwanga huo ni silaha imara ya kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Ujio wa mashine za kielekroniki za kutolea risiti za kodi (EFDs) nchini ni ukombozi wa ukusanyaji wa mapato ya nchi ambayo yalikuwa yakipotea na kulinyima taifa mapato kwa maendeleo yake, tofauti na mfumo wa zamani wa kukusanya mapato kwa risiti za vitabu vya mauzo.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) iliwahakikishia Wafanyabiashara na Watanzania kwa ujumla kuwa utaratibu wa kutumia Mashine za EFD ulianzishwa kwa lengo la kumrahisishia mfanyabiashara utunzaji wa kumbukumbu za biashara za kila siku pamoja na kuondoa usumbufu wakati wa ukadiriaji wa kodi. Kwa mantiki hiyo ni wajibu wa Serikali na taasisi inayosimamia mapato ambayo ni TRA kutoa elimu kwa wateja ambao ni wafanyabiashara wakubwa na wadogo juu ya mfumo mpya wa ukusanyaji kodi.

Dhamira ya TRA katika Mpango mkakati wake wa Nne wa kukusanya mapato nchini ni “Kurahisisha ulipaji wa kodi na kuyafanya maisha yawe bora”. Kwa dhamira hiyo, TRA imekuwa ikiendesha kampeni za kuwahamasisha walipa kodi na jamii kwa ujumla umuhimu wa kutoa na kudai risiti sahihi za mashine za kielekroniki za kutolea risiti za kodi (EFDs).

Kabla ya kuanza utekelezaji wa mfumo huu, elimu ilitolewa kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kupitia vyombo mbalimbali vya habari pamoja na semina ambazo zilitolewa kwa makundi mbalimbali ya wafanyabiashara.

Ni dhahiri kuwa elimu hiyo bado inaendelea kutolewa kwa njia mbalimbali ambapo kuhusu ununuzi wa mashine hizo kwa awamu ya pili, muda wa maandalizi ulisogezwa hadi Desemba 31, 2013 na taarifa ilitolewa na bado zinaendelea kutolewa kupitia vyombo vya habari.

Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa Sekta Binafsi inaendelea kutoa elimu kuhusu matumizi endelevu na faida za Mashine za EFD kwa wafanyabiashara na wanunuzi wa bidhaa na huduma mbalimbali za kijamii.

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.