Kikosi cha Israel cha kukabiliana na ugaidi kinatarajiwa kujiunga na juhudi za kuwatafuta zaidi ya wasichana 200 waliotekwa nyara nchini Nigeria na wanamgambo wa kundi la Boko Haram
Jeshi la Nigeria linafanya kila juhudi kuwatafuta wasichana hao ingawa limelaumiwa kwa kujikokota
Kundi hilo litajiunga na wataalamu wa Marekani,Uingereza na ufaransa ambao tayari wako nchini Nigeria.
Rais Goodluck Jonathan amesema kuwa kujiunga kwa
Israel katika operesheni hiyo ni wazi kwamba dunia nzima inaunga mkono
usakaji wa wasichana hao.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria amesema kuwa
uwepo wa wataalam wa Israel katika oparesheni hiyo huenda kukazua hisia
za kisiasa nchini Nigeria ambapo wasiwasi kati ya wakristo wanaoshi
kusini mwa taifa hilo na waislamu wanaoishi kazkazini huzua ghasia.
Awali Gavana wa jimbo la Borno Kaskazini
Mashariki mwa taifa hilo, eneo ambalo wasichana hao walitekwanyara
alisema kuwa ana habari kuhusu kule walipo wasichana hao.
habari na BBC swahili
No comments: