Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekahu amesema kuwa atawaachilia huru wasichana waliotekwa nyara iwapo tu wapiganaji wa kundi hilo wanaozuiliwa na serikali ya Nigeria wataachiliwa huru

Wasichana ambao kundi la Boko Haram liliwateka nyara
Katika kanda mpya iliyotolewa na kundi hilo, kiongozi huyo, amesema
kuwa wasichana hao waliweza kusilimu katika kipindi cha wiki nne
zilizopita tangu watekwe nyara.
Kanda hiyo inaonyesha zaidi ya wanawake miamoja
wakiwa wamevalia hijabu na kuswali. Abubaka Shekau anasema kuwa wanawake
hao ni wasichana waliotekwa nyara na kundi hilo.
Walitekwa nyara kutoka katika shule yao mjini Chibok, Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo
Rais wa Ufaransa amejitolea kuwa mwenyeji wa mkutano utakaotafuta njia za kupambana na Boko Haram.
No comments: