May 15 Kamata kamata bodaboda na bajaji mjini, Jiji lageuza biashara..!

Tangazo lililobandikwa na Jiji kusitisha zoezi la ukusanyaji wa tozo/vibali vya kuingia mjini na pikipiki.

-Baadhi
ya madereva wa pikipiki wanaozitumia kama vyombo vya usafiri binafsi
kwenda na kurudi kazini wakihoji juu ya mkanganyiko huo katika ofisi za
Jiji la Dar es Salaam, juzi. Hata hivyo hawakupata majibu zaidi ya
kukuta tangazo lililositisha upokeaji wa toza za kuingia mjini na
vibali.
ZOEZI la kupiga marufuku bodaboda na bajaji
zinazofanya biashara katikati ya Jiji la Dar es Salaam limegeuka
biashara kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam hasa kwa watumiaji wa
pikipiki hizo kwa ajili ya usafiri binafsi wa kawaida kwenda na kurudi
kazini, pamoja na makampuni yanayotumia chombo hicho cha usafiri.
Halmashauri ya jiji sasa imeanza kuwatoza watu
binafsi na makampuni yanayotumia chombo hicho shilingi 500 kwa siku kila
bodaboda inapoingia mjini wakidai ni tozo ya chombo hicho kupata idhini
ya kuingia mjini kwa kila siku.
No comments: