Sudan kusini Malumbano yameibuka
Mkataba wa amani uliotiwa saini ulipaswa kumaliza kabisa vita kati ya pande hasimu
Sasa Serikali na wapiganaji wa Sudan Kusini wanalaumiana kila upande
ukimshutumu mwenzake kuvunja makubaliano hayo yaliyosainiwa ijumaa.
Hata hivyo kiongozi wa waasi Riek
Machar anasema bado ameazimia kutekeleza makubaliano hayo licha ya
kwamba anasema serikali ya rais Salva Kiir inavunja mapatano hayo.
Machar amesema kuwa majeshi ya UPDF ya Uganda
ambayo yamekuwa yakivamia maeneo inayoyadhibiti haijaafiki mkataba
uliotiwa saini huko Adiss Ababa kati yake na Rais Salva Kiir.
Aidha msemaji wa jeshi la serikali, Kanali
Philip Aguer, amesema waasi hao wameshambulia maeneo ya serikali katika
mji wa Bentiu .
'Mazungumzo zaidi'
Upinzani umepinga madai hayo.
Machar ameiambia BBC kuwa angetaka mazungumzo
zaidi na serikali kuhusu hilo, lakini amesema anafahamu kuwa Rais hana
uwezo wa kudhibiti majeshi yote yanayopigana kwa upande mmoja na majeshi
ya serikali kama vile majeshi ya Uganda na wapiganaji kutoka Darfur.
Serikali ya Sudan Kusini pia imelaumu upande wa
waasi kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano saa chache tuu baada
ya mkataba huo kutiwa saini.
Makubaliano ya kusitisha mapigano yalitiwa saini
Ijumaa, na yalikusudiwa kumaliza vita vya miezi mitano ambavyo vimeuwa
maelfu ya watu na kulazimisha zaidi ya milioni moja kuhama makwao.
No comments: