Ads Top

KICHANGA CHATELEKEZWA USAGARA

Na Antony Sollo Mwanza
July 22, 2014.
KITOTO kichanga chenye umri wa miezi miwili kimetelekezwa katika maeneo ya Usagara Wilaya ya Misungwi Mkoani mwanza   barabara ya Kigongoferry kuelekea Sengerema na Geita.

Akizungumza na Tanzania daima Afisa mtendaji wa Kijiji cha usagara Raymond Mahumbi alisema kuwa tukio hilo lilitokea julai 21  majira ya saa 2:00 asubuhi huko Usagara ambapo alipewa taarifa za kutelekezwa kwa kichanga hicho ndipo alipokwenda katika eneo la tukio na kukuta kichanga hicho kikiwa kimetelekezwa katika nyumba ya Mapambano Wilson.

 Imedaiwa kuwa julai 21  majira ya saa 2:00 asubuhi  mama wa kichanga hicho alifika nyumbani kwa Mapambano na kuomba maji ya kunywa mara baada ya kunywa maji hayo, mtu aliyemhudumia alirudisha kikombe ndani na aliporudi hakuweza kumkuta mama wa kichanga hicho kwani alikuwa ametokomea kusikojulikana na kukiacha kichanga chake hicho sebuleni hapo.

“Mama wa kichanga hiki alifika hapa nyumbani akaniomba nimsaidie maji ya kunywa,nilimpatia na nilirudisha kikombe ndani nilikikuta kichanga hiki kikiwa peke yake kinalia na nilipojaribu kuchungulia huku na huku sikuweza kumuona mama huyo ndipo nilitoa taarifa kwa Afisa Mtendaji wa kijiji”alisema Mapambano .  

Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo walisema mama wa huyo amefanya kitendo kisichokubalika katika jamii hivyo wanannchi hao wamekilaani kitendo hicho kwa nguvu zote na kuomba kutoa ushirikiano kwa mtu yeyote atakayekuwa na taarifa za mama huyo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa,Jeshi la Polisi linamsaka mama huyo ili akipatikana aweze kufikishwa katika vyombo vya sheria kufuatia kitendo cha kikatili alichokifanya kwakuwa ni kitendo kisichokubalika katika jamii.
Mwisho

No comments:

UHURUTZ. Theme images by hanoded. Powered by Blogger.