KICHANGA CHATELEKEZWA USAGARA
Na
Antony Sollo Mwanza
July
22, 2014.
KITOTO kichanga chenye umri wa miezi miwili kimetelekezwa
katika maeneo ya Usagara Wilaya ya Misungwi Mkoani mwanza barabara ya Kigongoferry kuelekea Sengerema
na Geita.
Akizungumza na Tanzania daima Afisa mtendaji wa Kijiji cha
usagara Raymond Mahumbi alisema kuwa tukio hilo lilitokea julai 21 majira ya saa 2:00 asubuhi huko Usagara
ambapo alipewa taarifa za kutelekezwa kwa kichanga hicho ndipo alipokwenda
katika eneo la tukio na kukuta kichanga hicho kikiwa kimetelekezwa katika
nyumba ya Mapambano Wilson.
Imedaiwa kuwa julai
21 majira ya saa 2:00 asubuhi mama wa kichanga hicho alifika nyumbani kwa
Mapambano na kuomba maji ya kunywa mara baada ya kunywa maji hayo, mtu
aliyemhudumia alirudisha kikombe ndani na aliporudi hakuweza kumkuta mama wa
kichanga hicho kwani alikuwa ametokomea kusikojulikana na kukiacha kichanga chake
hicho sebuleni hapo.
“Mama wa kichanga hiki alifika hapa nyumbani akaniomba
nimsaidie maji ya kunywa,nilimpatia na nilirudisha kikombe ndani nilikikuta
kichanga hiki kikiwa peke yake kinalia na nilipojaribu kuchungulia huku na huku
sikuweza kumuona mama huyo ndipo nilitoa taarifa kwa Afisa Mtendaji wa
kijiji”alisema Mapambano .
Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo walisema mama wa huyo amefanya kitendo kisichokubalika katika jamii hivyo wanannchi hao wamekilaani kitendo hicho kwa nguvu zote na kuomba kutoa ushirikiano kwa mtu yeyote atakayekuwa na taarifa za mama huyo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na
kusema kuwa,Jeshi la Polisi linamsaka mama huyo ili akipatikana aweze
kufikishwa katika vyombo vya sheria kufuatia kitendo cha kikatili alichokifanya
kwakuwa ni kitendo kisichokubalika katika jamii.
Mwisho
No comments: