Kanda ya video inayomuonyesha mtu anayedaiwa kuwa kiongozi wa kundi la Boko Haram imetolewa akikana madai ya jeshi kwamba amefariki
Katika kanda hiyo, Abubakr Shekau
anasema kuwa wapiganaji wake waliitungua ndege ya wanajeshi wa angani
iliotoweka wiki tatu zilizopita.
Wiki iliopita jeshi lilidai kuwa
mtu anayejionyesha katika kanda ya video ya Boko Haram aliuawa mwezi
Agosti 2013 likadai kwamba huenda Shekue amefariki.
Wachanganuzi wametilia shaka kuhusu uthabiti wa madai hayo ya jeshi.
Mwandishi wa Nigeria Ahmad Salkida, ambaye ana mawasiliano mazuri na
Boko Haram alisema kuwa katika mtandao wake wa Twitter wiki iliopita ana
hakika kwamba Shekue yu buheri wa afya na kwamba hajafariki.
Haijabainika ni lini ama wapi kanda hiyo iliopatikana na shirika la habari la AFP ilitengenezwa.
lakini
muhariri wa Idhaa ya BBC Hausa, Mansur Liman, amesema kuwa mtu
aliyezungumza katika kanda hiyo ya video alikuwa Abubakr Shekue yule
yule anayeonekana katika kanda nyengine za video za kundi la Boko Haram.
Habari na BBCswahili.com
No comments: